Sibuka FM

Takukuru  Simiyu  yaokoa  milioni 500 za  mfanyabiashara

18 August 2023, 10:05 am

Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Simiyu Aron Misanga akitoa taarifa kwa Waandishi wa habari ambao hawapo pichani kwa Robo ya Nne (April – Juni ) kwa mwaka wa Fedha 2022/2023

TAKUKURU mkoa wa Simiyu imeokoa mamilioni ya fedha za mfanyabiashara ambaye mali zake zingepigwa mnada kwa bei ya kutupwa.

Na Nicholaus Machunda

Taasisi  ya  Kuzuia  na  Kupambana  na  Rushwa nchini TAKUKURU mkoa  wa  Simiyu  imefanikiwa  kudhibiti  upotevu  wa  zaidi ya  Shilingi  milioni mia tatu  katika  mnada  haramu  wa  ghala  na  nyumba tatu  za  kuishi   mali  ya  mfanyabiashara  anayejulikana  kwa  jina  la  Sibu  Nsugi  Manabu mkazi  wa  wilaya  ya  Bariadi  mkoani   hapa.

Akitoa  taarifa  ya  robo  ya  nne  ya  mwaka  wa  fedha  2022/2023 ( April – Juni )  kwa  waandishi  wa  habari,   Naibu  Mkuu  wa  Takukuru  Mkoa  wa  Simiyu   Aron  Misanga  amesema  kuwa   thamani   ya  ghala  hilo  ni  zaidi  ya  Shilingi  milioni  mia tano  lakini  lilikusudiwa  kuuzwa   chini  ya  shilingi  milioni mia mbili.

Sauti ya Aron Misaga Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Simiyu

Naibu  Mkuu  wa   Takukuru  huyo  amefafanua  kuwa    mfanyabiashara  huyo  alikopa  fedha  kwenye  benki  na  kushindwa  kurejesha  hivyo  kupelekea  mali  zake  kukamatwa  na  kutaka  kuuzwa  kwa  mnada  wa  hadhara  ulioendeshwa  na  kampuni  ya  Bani  Investment  Limited  hali  ambayo  utaratibu  haukufuatwa  na  kupelekea  Takukuru  kuingilia  kati.

Sauti ya Aron Misaga Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Simiyu

Katika  hatua  nyingine  Taasisi  ya  Kuzuia  na  Kupambana  na  Rushwa  Mkoa  wa  Simiyu  imefuatilia  Miradi  Ishirini  na  tano (25)  ya  Maendeleo  yenye  thamani  ya  Zaidi  ya  Shilingi  Bilioni  6. 8  katika  Sekta  za  Elimu,  Afya,  Maji  na  Barabara  kwa  lengo  la  Kudhibiti  Ubadhilifu   wa  Fedha  za   Umma.

Sauti ya Aron Misaga Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Simiyu

Aidha   TAKUKURU  Mkoa  wa  Simyu  inaendelea  na  Mikakati  ya  Kuzuia  Rushwa  katika  Eneo  la  Ukusanyaji  wa  Mapato  kwa  kutoa  Elimu  kwa  makundi  mbalimbali   rasmi  na  yasiyo  rasmi,  Sehemu  zenye  mikusanyiko  ya  Watu  pamoja  na  Vipindi  vya  Radio  Jamii    Sibuka  fm.

Sauti ya Aron Misaga Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Simiyu

      

Baadhi ya Watumishi wa Taasisi ya Takukuru Mkoa wa Simiyu wakifuatilia taarifa