Sibuka FM
Sibuka FM
12 May 2026, 19:02

Lazima mkulima ashiwe mkono kama mtoto mdogo anavyoshikwa mkono wakati wa kuvukishwa barabarani, ndio maana serikali inamhudumia kuanzia pembejeo hadi kwenye masoko, tunatamani heshima ya pamba urudi. ” Agrey Mwanri -balozi wa pamba tanzania “
Imeelezwa kuwa Serikali ya awamu ya sita imeendelea kuweka mikakati mathubuti ya kuhakikisha inasaidia wakulima wa zao la Pamba na kuleta tija kwa kuongeza uchumi wa mtu mmoja mmoja
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Igunga Mhe Sauda Mtondoo aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa Tabora Mhe Paul Chacha wakati wa Uzinduzi wa Msimu wa ununuzi wa zao pamba uliofanyika katika kijiji cha mwamashimba wilayani hapo ambapo bei elekezi ya Serikali kwa msimu huu ni shilingi 1,240 kwa Kilo moja
Kwa upande wake Kaimu mwenyekiti wa Bodi ya Pamba Tanzania –TCB na Balozi wa Pamba nchini Agrey Mwanri amesema kuwa ni wakati muafaka wa kuleta heshima ya zao la Pamba na kuacha alama kwa wakulima wanaolima zao hilo

Anamringi Macha ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu amesema kuwa mkoa wa simiyu umekuwa kinara kwa uzalishaji huku matarajiwa katika msimu huu wa 2026/2027 ni kuvuna pamba ya zaidi ya kilo milioni 177 sawa na asilimia 60 ya pamba yote nchini itayonunuliwa
Nao baadhi ya wadau wa zao la Pamba wakawahakikishia wakulima uhakika wa Fedha baada ya kuuza pamba yao huku wakala wa vipimo akiwaonya wale wanaofanya udanganyifu wa kuchakachua mizani kwa lengo la kuwaibia wakulima

