Sibuka FM
Sibuka FM
12 December 2024, 15:51

Wadau na wanaharakati wa haki za binadamu Duniani na Nchini Tanzania wameendelea na harakati za kuhakikisha kuwa usawa kwa wote unafikiwa,licha yakuwepo na wimbi la taarifa za ukatili wa kijinsia unaoripotiwa kwenye maeneo mengi Nchini na Duniani kwa ujumla.
Na,
Alex Sayi
Halmashauri Wilayani Maswa Mkoani Simiyu imebainisha kuwa vitendo vya ukatili wa kijinsia vinaonyesha kupungua kutoka matukio(671)mwaka 2023 hadi kufikia matukio(591)2024.
Kauli hiyo imetolewa na Afisa Ustawi wa jamii Wilayani hapa Bi,Lilian Clement kwenye kilele cha maadhimisho ya siku(16) za kupinga ukatili wa kijinsia yaliyofanyikia kijiji cha Mbugamita kata ya Senani Wilayani hapa.

Dr,Stanford Kaserwa Meneja mradi wa (React-in)akizungumza kwenye warsha hiyo amesema kuwa shirika limeendelea kuwahamasisha vijana wa kiume na kinababa kushiriki mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia


Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa,Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Bw,Athmani Zahoro Kalaghe amesema kuwa Serikali ilishatunga Sheria na miongozo, hivyo jamii inapaswa kutoa taarifa pindi tu wanapobaini kuwepo kwa matukio hayo.

