Sibuka FM

54 wabatizwa makambi ya mtaa wa Luguru Ginnery Itilima

8 August 2026, 12:51

Pichani mwenye suti na aliyeshika kipaza sauti ni mchungaji ,Daniel Gamal Budo wa mtaa wa Gasuma akiendelea kufundisha neno kwa wabatizwa wanaoonekana nyuma yake katika makambi ya mtaa wa Luguru Ginnery Picha na Daniel Manyanga

“Matamanio yetu ni kuona watu wanabadili nia na kumgeukia Mungu maana mambo ya kidunia mara nyingi mwisho wake huwaga ni mbaya sasa ni muda mwafaka wa kuihubiri injili ya Bwana kwa watu wote”.

Na,Daniel Manyanga

Watu 54 wamebatizwa katika makambi ya mtaa wa Luguru Ginnery Kanda ya Luguru Ginnery wilayani Itilima mkoani Simiyu kufuatia kukubali kuwa Yesu Kristo ni mwokozi wa maisha yao.

Akizungumza na Sibuka Fm wakati wa kuhitimisha sikukuu ya vibanda katika makambi hayo Kanda ya Luguru Ginnery mchungaji wa kanisa la waadventista wasabato mtaa wa Gasuma ,Daniel Gamal Budo amesema kuwa ni furaha kubwa kuona watu wameamua kuachana na maisha ya dunia hivyo kumpokea Yesu ili awe kiongozi wao.

Mchungaji Gamal amewakumbusha wale wote waliopokea ubatizo wa maji marefu katika makambi hayo kusonga mbele kwa nguvu katika kuifanya kazi ya Mungu bila kujali jamii itawaonaje kutokana na ubatizo huo.

Sauti ya mchungaji Daniel Gamal Budo

Jacob Mwampamba ni Mchungaji wa kanisa la waadventista wasabato mtaa wa Somanda wilayani Bariadi ametoa wito kwa makanisa ya mtaa wa Luguru Ginnery kuendelea kuwapa masomo wale wote waliobatizwa ili kuendelea kukaa kwenye mwokovu.

Sauti ya mchungaji, Jacob Mwampamba akitoa wito kwa makanisa kuendelea kuwalea wale wote waliopokea ubatizo
Pichani ni mchungaji Jacob Mwampamba wa mtaa wa Somanda wilayani Bariadi akiwa katika makambi ya mtaa wa Luguru Ginnery Picha na Daniel Manyanga

Ezekiel Magembe ni mmoja wapo wa vijana waliobatizwa katika makambi hayo amewaomba vijana wengine kuachana na anatha za dunia na kumgeukia Yesu Kristo aliyekufa msalabani kwa ajili ya watu wenye dhambi na kufanyika mkombozi hivyo wabatizwe.

Sauti ya Ezekiel Magembe mmoja wa vijana waliobatizwa kwa maji marefu
Pichani ni mchungaji ,Daniel Gamal Budo akiendelea na ubatizo katika makambi ya mtaa wa Luguru Ginnery Picha na Daniel Manyanga

Kwa upande wake meneja wa makambi kanda ya Luguru Ginnery, Manjale Magembe amesema kuwa katika makambi hayo jumla ya makanisa manne yanayounda mtaa wa Luguru Ginnery yameshiriki kwenye makambi hayo yaliyoambatana na matembezi.

Sauti ya meneja wa makambi kanda ya Luguru Ginnery, Manjale Magembe
Kwenye picha aliyeshika kipaza sauti ni meneja wa makambi kanda ya Luguru Ginnery, Manjale Magembe akizungumza jambo kwenye makambi ya mtaa wa Luguru Ginnery Picha na Daniel Manyanga
Picha katika matukio mbalimbali wakati wa makambi ya mtaa wa Luguru Ginnery Picha na Daniel Manyanga