Sibuka FM

Serikali yatangaza bei elekezi ya pamba, wakulima watoa ya moyoni

12 May 2026, 18:00

uzinduzi wa msimu wa pamba 2026/2027 katika kijiji cha mwamashimba wilaya ya Igunga mkoa wa
Tabora. Picha na Nicholaus Machunda

Yamezungumzwa mengi na watangulizi wangu lakini naomba nikuongezee machache mgeni rasmi kuwa hapa Igunga kutajengwa kiwanda kiubwa cha kuchakata pamba kabla ya mwaka huu haujaisha maana tayari tumeshapata eneo “Renatus Luneja Mkurugenzi mkuu wa Bodi ya pamba Tanzania-TCB “

Serikali  kupitia  Bodi ya  Pamba  Tanzania  TCB  imetangaza  bei  elekezi  ya ununuzi wa zao la  Pamba  kwa  msimu  wa  2026/ 2027  ambapo   Pamba  ya daraja la kwanza itanunuliwa  kwa  shilingi 1,240  kwa  kilo moja  huku  pamba  ya daraja la pili  ikinunuliwa  kwa  shilingi  620  kwa  kilo moja.

Bei hiyo elekezi  imetangazwa  na  Mkuu wa  Wilaya ya  Igunga  Mhe  Sauda  Mtondoo  kwa  niaba ya  Mkuu  wa  Mkoa  wa  Tabora  Mhe  Paul  Chacha  wakati  wa  Uzinduzi  wa  msimu wa ununuzi  wa  pamba uliofanyika  katika  kijiji  cha  Mwamashimba  Wilayni  Igunga  Mkoani  hapo

Hii hapa sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Igunga mhe Sauda mtondoo
aliyevaa skafu ni mkuu wa wilaya ya Igunga mhe Sauda Mtondoo akishuhudia mzani wa kupimia pamba wakati wa Uzinduzi wa msimu

Kwa  upande  wake  Mkurugenzi  Mkuu wa Bodi ya  Pamba  Tanzania  Renatus  Luneja  amesema  kuwa    kwakutambua  umuhimu wa  Wilaya ya  Igunga Serikali  itaendelea  kuboresha  mazingira kwa  kujenga  kiwanda  cha  kuchakata  mbegu kabla ya  mwaka  huu  kuisha

hii hapa ni sauti ya mkurugenzi mkuu wa Bodi ya pamba Tanzania -Renatus Luneja

Baadhi ya  wakulima  waliozungumza  na  Sibuka  wakatoa  maoni  yao  kuhusu  bei elekezi  iliyotangazwa  na  Serikali  huku  wito  ukitolewa  kwa  wakulima  kuhakikisha  wanazingatia  utunzaji  wa  Pamba  wakati  wa  Uvunaji  ili  kuepuka  kuchafua  pamba  hali itayopelekea  kushuka  kwa  thamani ya  zao hilo

hizi hapa baadi ya sauti za wadau wa pamba wakizungumza wakati wa uzinduzi

Bei ya  pamba imeongezeka  ikilinganishwa  na bei ya  msimu  uliopita  wa  2025/2026 ambapo kilo moja ya  pamba  ilinunuliwa  shilingi 1,150  na kwa  msimu huu  wa  2026/2027 kilo moja ya  pamba  itanunuliwa  kwa  shilingi  1,240 sawa na ongezeko la shilingi 90 kwa kilo moja

balozi wa Pamba Tanzania Agrey Mwanri akizungumza wakati wa uzinduzi wa msimu wa pamba-Igunga
Mhe Sauda Mtondoo mkuu wa wilaya ya Igunga akizungumza wakati wa uzinduzi