Sibuka FM

Viongozi  wa Amcos  na  BBT  wafundwa  kuhusu usafi na Ubora wa Pamba

20 May 2026, 00:23

Picha: aliyeshika mic(katikati) ni Thomas Masanja Shilabu mkuu wa divisheni ya kilimo na mifugo wilaya ya meatu akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo, kushoto kwake ni Bi, Sharifa Salumu na kulia kwake ni Bi Penina Range ambao ni wataalamu wa maabara kutoka Bodi ya Pamba Tanzania. Picha na Nicholaus Machunda

Kwasasa wilaya ya Meatu tumepiga marufuku uvunaji wa pamba kwa kutumia vikundi vya ngoma na mziki maana havizingatii kanuni bora za pamba hali inayopelekea uchafuzi wa pamba wakati wa uvunaji ” Thomas Shilabu afisa kilimo wilaya ya meatu “

Viongozi wa vyama vya msingi vya ushirika (AMCOS ), maafisa kilimo wa program  ya Jenga  kesho iliyo bora  (BBT)  pamoja na mampuni ya ununuzi wa zao pamba Wilayani  Meatu Mkoani Simiyu wamepewa mafunzo ya  namna ya kusimamia  usafi na ubora katia zao la pamba ili kuleta tija katika soko la  kimataifa

Hayo yameelezwa  na  mkuu wa divisheni  ya kilimo na  mifugo   wilayani hapo  ndugu  Thomas Masanja Shilabu   kwa niaba ya  Mkuu wa  wilaya  ya  meatu  Mhe  Fauzia  Hamidu Ngatumbura na  kusema  kuwa wakulima wamekuwa  wakiharibu ubora  kwa  kutokuzingatia kanuni nzuri  za  uvunaji  na  badala yake kutumia ngoma na mziki maarufu kwa  jina la  kumba kumba hali inayopelekea kuharibu  pamba

Bonyeza hapa kusikiliza sauti ya Thomas Shilabu -Afisa kilimo wilaya ya meatu

Mkuu huyo wa divisheni ya  kilimo na mifugo  amesema  kuwa  sheria  za pamba  zipo hivyo viongozi wa  vyama  vya  Amcos  na  BBT   wazisimamie ili pamba  itakayonunuliwa  iwe  safi na  bora  huku akieleza matarajio ya  kilo zitakazovunwa  katika msimu  wa  huu  wa  2026/2027 ni makubwa  ukilinganisha na  msimu uliopita  wa  2025/2026

Hii hapa sauti ya Thomas Shilabu -Afisa kilimo wilaya ya meatu
aliyeshika mic ni Sharia Salum afisa kutoa bodi ya pamba akizungumza wakati wa mafunzo

Penina  Range  na  Sharifa  Salum ni  wataalamu wa  maabara  katika  kitengo cha  Usafi na  ubora  wa pamba   kutoka  Bodi ya  Pamba Tanzania  -TCB   wamesema  kuwa lengo la kutoa  Semina  hizo ni kuhakikisha  usimamizi  wa usafi  na  ubora wa pamba unaimarishwa kupitia kwa viongozi wa Amcos, BBT  wasimamizi wa ununuzi  hasa katika  msimu  huu  wa  soko

sauti ya Penina Range na Sharifa Salum kutoka TCB wakizungumza wakati wa mafunzo

Aidha  wa  upande  wake mkaguzi  wa Pamba  wilaya ya  meatu   Hemed  Kabeya  amesema  kuwa  hawatawavumilia  viongozi wote  watakaofanya  ubadhilifu  kwa  wakulima watawaondoa mara  moja  huku  akiwataka  kufanya  kazi kwa ueledi na  uadilifu ili kuepuka  kuingia kwenye migogoro hiyo

Hii hapa ni sauti ya Hemed Kabeya mkaguzi wa Pamba wilaya ya Meatu

Nao viongozi wa  Amcos na maafisa kilimo wa  BBT  wamesema  watahakikisha  wanayafanyia kazi yale yote  waliyoelekezwa kwenye  Semina  ili pamba  itakayonunuliwa iwe  safi  na bora na ifae katika ushindani wa  soko la  Dunia  hivyo hawatakubali kununua  pamba chafu

sauti za viongozi wa Amcos na BBT wakizungumza baada ya mafunzo
picha za matukio mbalimbali wakati wa mafunzo ya Usafi na ubora wa pamba yaliyofanyika wilayani Meatu mkoani Simiyu