Sibuka FM

Maswa : Wenyeviti wa Vitongoji  walia na TARURA kuhusu ubovu wa barabara

5 June 2026, 22:19

Picha: aliyesimama ni Bi Caroline Shayo -Mwenyekiti wa mamlaka ya mji mdogo Maswa, kulia kwake (mwnye miwani aliyekaa ), Bi Veronica Mbiha – Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu Mamlaka ya mji mdogo Maswa wakati wa Kikao cha Baraza la mamlaka ya mji huo robo ya tatu ya mwaka wa Fedha 2025/2026. Picha na Nicholaus Machunda

Kila mmoja akitimiza wajibu wake katika kufanya kazi hautakuwa na migogoro yoyote, Lakini kwasababu tunafanya kazi kwa matakwa ya watu fulani ndio maana inafikia hatua ya mizozo kama hii ” Bi Caroline Shayo -Mwenyekiti wa mamlaka ya mji mdogo Maswa “

Wenyeviti wa vitongoji  vinavyounda mamlaka ya  mji mdogo  Maswa, Mkoani  Simiyu wamelalamikia  ubovu wa  barabara  kutopitika  hasa kipindi hiki baada ya mvua za masika kuziharibu licha  ya  kuwa  vitongoji  hivyo kuwa   Maswa  mjini hali inayopelekea  ucheleweshwaji  wa  maendeleo.

Hayo  yamesemwa  na  wajumbe  hao  katika kikao cha  baraza la mamlaka ya mji mgodo  kwa  robo ya  tatu  ya  mwaka wa  fedha 2025/2026 kilichofanyika  katika  Ukumbu wa  ofisi za  mamlaka  zilizopo mtaa wa  Ujenzi  maswa mjini

Bonyeza hapa kusikiliza sauti za wajumbe wa baraza la mamlaka ya mji mdogo Maswa

Wajumbe  hao  wamesema  kuwa  Wakala wa  barabara za  Vijijini – TARURA  wamekuwa  hawashirikishi viongozi wa vijiji na  vitongoji wakati wa  kubaini vipaumbele vya  barabara   katika  maeneo  hali  inayopelekea  kurudia  barabara zile zile ambapo zinapitika  muda  wote

Bonyeza hapa kusikiliza sauti za wajumbe wa baraza la mamlaka ya mji mdogo Maswa wakichangia hoja
wajumbe wa baraza la mamlaka ya mji mdogo Maswa wakifuatilia hoja kwenye makabrasha

Hali  hiyo ilisisitizwa  na  Mwenyekiti wa  Mamlaka  ya  mji  huo   Mhe, Caroline  Shayo  na  kusema  kuwa  wamekuwa  wakiacha  kutengeneza  barabara  zenye  vipaumbele  na  ambazo  hazipitiki  kabisa  hivyo kabla ya  kuanza  matengenezo  washauriane  na  Diwani husika  au viongozi wa  vitongoji   husika

sauti ya Caroline Shayo – Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mji mdogo Maswa akizungumzia ubovu wa barabara

Akijibu  hoja  za  wajumbe  hao, Kaimu  meneja  wa  Tarura  Wilaya ya  Maswa  Mhandisi  Baraka  Libungo amesema  kuwa  tayari  tarura  imetenga  fedha  kwa  ajili ya  matengenezo ya  barabara korofi ili zipitike  na  kuchochea  uchumi wa  Wananchi  wa  Maswa

sauti ya Mhandisi Baraka Libungo – Kaimu meneja Tarura wilaya ya Maswa

Aidha  mwenyekiti wa  Mamlaka  hiyo  Bi  shayo  akazungumzia  suala  ya  mzabuni  wa  kukusanya  taka katika  mji wa Maswa  kuwa  mzabuni  huyo  hafai  na  ameshindwa  kukidhi   vigezo na matakwa  ya  kukusanya  taka  kama walivyotarajia  hivyo  mamlaka  haitaendelea  kufanya  kazi  nae.

sauti ya Caroline Shayo – Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mji mdogo Maswa akizungumzia sakata la mzabuni wa usafi mji wa maswa