Sibuka FM
Sibuka FM
5 May 2026, 00:16

Zoezi hili ili lifanikiwe liwashirikishe hadi viongozi wa ngazi za chini kama vile wenyeviti wa vijiji na Vitongoji na mabalozi ili kuondoa upotoshaji unaojitokeza ” Mhe Anna Gidarya -Kaimu DC Maswa “
Zoezi la Utoaji wa Chanjo ya Polio awamu ya pili Wilayni Maswa, Mkoani Simiyu itatolewa kuanzia tarehe 7 hadi 10 mwezi huu wa tano ambapo mkakati wa serikali ni kupita nyumba kwa nyumba ili kuhakikisha watoto wote wanafikiwa na zoezi hilo
Hayo yamesemwa na Afisa Afya Mkoa wa Simiyu Bashiri Salum wakati wa kikao kilichowakutanisha wadau mbalimbali chenye lengo la uhamasishaji wa chanjo hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa Wilaya.

Akitoa taarifa kwa Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya Christopher Msaghae amesema kuwa Wilaya tayari imepokea Chanjo ya Polio zaidi ya dozi laki mbili kwa ajili ya utekelezaji wa zoezi hilo
Kwa Upande wake Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Maswa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Itilima Mhe Anna Gidarya amesema kuwa zoezi hili lihusishe viongozi wa ngazi za chini wakimo wenyeviti wa vijiji na vitongoji na mabalozi ili kuondoa Upotoshaji huku suala la kutoa elimu ya faida ya chanjo hiyo kabla ya kuchanja akilisisitiza zaidi
Baadhi ya wajumbe wa kikao hicho, Shekhe wa Wilaya ya Maswa Shehke Issa Eliasa, katibu wa waganga wa Tiba asili ndugu Potini Shiri na mwenyekiti wa Mamlaka ya mji mdogo Maswa Bi Caroline Shayo wakaahidi kutoa ushirikiano wakati wa utekelezaji wa zoezi la utoaji wa chanjo hiyo
Kikao hicho kimehudhuriwa na wawakilishi wa makundi mbalimbali wakimo, Viongozi wa Dini, viongozi wa tiba asili, Wazee maarufu , makundi maaalumu, walimu wakuu, kamati ya afya ya msingi ya wilaya na viongozi wa kisiasa



Picha za wadau mbalimbali wakiwa katika kikao cha uhamasishaji wa chanjo wilayani Maswa