Sibuka FM

Mhandisi  Kundo atangaza rasmi  kugombea  Ubunge Jimbo la Bariadi Vijijini

5 May 2025, 14:46

Mbunge wa Jimbo la Bariadi Mhandisi Kundo Mathew akitoa taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya ccm ya 2020/2025 kwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu maalumu. Picha na Nicholaus Machunda

Ninatangaza rasmi kugombea nafasi ya Ubunge katika Jimbo la Bariadi Vijijini endapo Rais ataridhia kupitia Tume huru ya Uchaguzi Jimbo kugawanywa na kuwa mawili (Bariadi Mjini na Bariadi Vijijini) basi mimi nitagombea vijijini “Mhandisi Kundo Mathew “

Mbunge  wa Jimbo  la  Bariadi na Naibu  waziri  wa  Maji  Mhandisi   Kundo  Mathew  ametangaza  rasmi  kugombe nafasi ya Ubunge  katika  Jimbo  la  Bariadi vijijini   endapo  mchakato  wa  kuligawa  jimbo  hilo  utakamilika

Mhandisi  Kundo  ametangaza  dhamira  hiyo  wakati  wa  Uwasilishaji  wa  taarifa ya  Utekelezaji wa  Ilani ya  Chama  cha  Mapinduzi –ccm   ya  2020/2025   kwenye  Mkutano  Mkuu   Maalumu  wa  ccm  katika  Jimbo  la  Bariadi   uliofanyika  katika  shule  ya  Msingi  Bariadi  alliance

sauti ya Kundo Mathew Mbunge wa Jimbo la Bariadi akitangaza kugombea Bariadi Vijijini

Aidha  Mhandisi  Kundo amesema  kuwa  katika utekelezaji  wa  Miaka mitano  ya  Ilani  ya  ccm , Serikali  ya  awamu  ya  Sita  chini  ya  Rais  Mhe  Dkt  Samia  Suluhu  Hasan  imefanya  mambo  makubwa  katika  Sekta  za  Afya,  Elimu,   Maji, Barabara , Umeme na  Kilimo  ukilinganisha  na  hapo  awali  wakati  anachaguliwa  kuwa  mwakilishi  wa  Wananchi  katika  Jimbo  hilo

sauti ya Kundo Mathew Mbunge wa Jimbo la Bariadi akielezea mafanikio katika jimbo lake
Wajumbe wa Mkutano Mkuu maalumu wa Usomaji wa Ilani ya ccm wakiwa makini kusikiliza

Leila  Burhan  ni Mjumbe  wa  Kamati  Kuu  ya  ccm  Taifa  ndiye alikuwa Mgeni  rasmi ,  amewaomba  wana  Bariadi  kumuunga  mkono na  kuumpa  sapoti  Mhandisi  Kundo  muda  utakapofika  wa  kwenda  kugombea  Ubunge  kwa  Jimbo  lolote  katika   Wilaya  ya  Bariadi

sauti ya Leila Burhan -mgeni rasmi na Mjumbe wa kamati kuu ya ccm Taifa

Akimkaribisha  Mgeni  rasmi,  Mwenyekiti  wa  ccm  Mkoa  wa  Simiyu  Ndugu  Shemsa  Mohamed  amesema  kuwa  kwa  masrahi  mapana  ya  Bariadi  wameomba  Jimbo  ligawanywe ili  kusogeza  huduma  kwa  wananchi  kwani  kwa  sasa  Jimbo  lina  kata  31 hivyo ni  kubwa  mno katika  kulihudumia

sauti ya Shemsa Mohamed- Mwenyekiti wa ccm Mkoa wa Simiyu

Akitoa  salamu  za  Serikali, Mkuu  wa  Mkoa  wa  Simiyu  Mhe  Kenani  Kihongosi amesema  kuwa  Mkoa  umepokea  Fedha  nyingi  kwa  ajili  ya  utekelezaji  wa  Miradi  ya  Maendeleo   inayotekelezwa  katika  maeneo  mbalimbali  ya  Mkoa

sauti ya RC Simiyu Mhe, Kenani Kihongosi akitoa salamu za Serikali