Sibuka FM
Sibuka FM
3 March 2025, 12:36

Halmashauri Wilayani Maswa Mkoani Simiyu imeendelea na adhima yake ya kuhakikisha inaongeza ukusanyaji wa mapato kwa kuanzisha vyanzo vipya vya mapato kwa lengo la kuharakisha maendeleo Wilayani hapo
Na, Alex Sayi-Maswa Simiyu.
Halmashauri wilayani Maswa mkoani Simiyu imeanzisha gulio na mnada mpya wa mifugo kwa lengo la kuchochea maendeleo kwa wananchi na kuongeza wigo wa ukusanyaji wa mapato
Hayo yamesemwa na mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Bw,Maisha Mtipa wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani la robo ya pili,lilioketi feb,27/2025.

Aidha akizindua mnada huo katibu tawala wa Wilaya ya Maswa Mkoa wa Simiyu,Bw,Athuman Kalaghe amewapongeza madiwani kwa uamuzi huo,huku akitoa maelekezo juu ya usimamizi wa mnada huo

Kwa upande wake mkuu wa divisheni ya kilimo na uvuvi,Bw,Robert Urasa amesema kuwa mnada huo umegharimu zaidi ya Sh.Mil,34
