Sibuka FM
Sibuka FM
22 May 2026, 18:02

Hatutawavumilia viongozi wote watakaofanya udanganyifu wa uchezea (kuchakachua) mizani kwa lengo la kuwaibia wakulima, Lakini pia hatutawavumilia wakulima wataoharibu pamba kwa kuweka Maji, mchanga au Mafuta ya kenge hatua kali za kisheria zitachukuliwa ikiwemo kufungwa Jela. “Ndinda Antony – Mkaguzi wa Pamba wilaya ya Bariadi “
Serikali kupitia Bodi ya Pamba Tanzania –TCB imekuja na suluhisho kwa wanaochezea mizani ya kupimia pamba kwa lengo la kuwaibia wakulima wa zao hilo maana nia ya Serikali ni kuinua kipato cha mkulima mmoja na taifa kwa ujumla
Hayo yamesemwa na mkaguzi wa pamba Wilaya ya Bariadi Mkoa wa Simiyu ndugu Ndinda Antony wakati akiongea na viongozi wa Amcos katika kata ya Dutwa wilayani hapo wakati wa utoaji wa wa Semina ya usafi na ubora wa pamba iliyoandaliwa na bodi ya Pamba Tanzania
Ndugu Ndinda ameongeza kuwa katika kuhakikisha ubora wa pamba unasimamiwa, sheria ipo wazi wa wataofanya udanganyifu wa kuweka maji, kuweka michanga au mafuta ya kenge kwenye pamba watachukuliwa sheria ikiwemo kufungwa jela au kulipa faini au vyote kwa pamoja

Kwa upande wao maafisa kilimo wa program ya Jenga kesho iliyo bora – BBT wamesema watatumia vyema taaluma na maarifa yao waliyopata kwa kuwashauri vyema wakulima kufuata kanuni bora za kilimo ikiwemo uvunaji sahihi wa pamba ili kuweza kuthibiti ubora wa pamba
Nao baadhi ya viongozi wa AMCOS walioshiriki mafunzo hayo ya Usafi na ubora wa Pamba kutoka wataalamu wa maabara kitengo cha usafi na ubora wa pamba wamesema wataenda kusimamia kikamilifu ubora wa pamba kwa kufuata sheria, kanuni na maagizo waliyopewa
Bodi ya Pamba Tanzania kupitia maafisa wa kitengo cha maabara na usafi wa pamba wanapita katika maeneo mbalimbali ya mikoa inayolima zao hilo la pamba kwa lengo la kutoa elimu ya utunzaji, Usafi na ubora wa Pamba.


