Sibuka FM
Sibuka FM
17 September 2026, 12:01

“Katika shughuli zenu jitahidini sana kuwa walinzi wa amani katika jamii yetu kuweni sehemu ya kufichua uhalifu na wahalifu wenyewe na siyo kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani”.
Na,Daniel Manyanga
Mkuu wa mkoa wa Simiyu ,Said Mtanda amewataka waganga wa tiba asili na mbadala mkoani humo kutumia vilinge vyao kufichua watu wote wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu ili wachukuliwe hatua kali za kisheria jambo litakalosaidia kuimarisha ulinzi na usalama katika jamii na siyo kupiga ramli chonganishi.
Mtanda ametoa wito huo wakati akizungumza na waganga wa tiba asili na mbadala wa mkoa wa Simiyu katika kikao kilichofanyika mjini Bariadi, ambapo amesema kuwakuna umuhimu mkubwa kwa kundi hilo kushiriki kikamilifu kufichua wahalifu ili kupunguza vitendo viovu ndani ya jamii zetu.
Awali akizungumza katika kikao hicho kaimu katibu wa waganga wa tiba asili mkoa wa Simiyu, Bunani Jackson ameeleza changamoto zinazowakabili katika shughuli zao na kuiomba serikali kuzifanyia kazi.
Akijibia changamoto hiyo mkuu wa mkoa wa Simiyu, Said Mtanda akaeleza hatua zitakazofanywa na serikali ya mkoa huo katika kushughulikia changamoto za waganga hao.