Chai FM

Recent posts

30 September 2023, 3:04 pm

Taulo zimekuwa mkombozi kwa wanafunzi wa kike mashuleni

wanafunzi wa shule ya sekondari tukuyu wilayani Rungwe wakiwa wanapokea taulo[picha na lennox mwamakula] jamii imetakiwa kuendelea kumsaidia mtoto wa kike ili aweze kuondokana na vikwazo vinavyoweza kumkwamisha kutimiza ndoto zake RUNGWE-MBEYA Na lennox mwamakula Jumla ya pisi elfu ishirini…

21 September 2023, 4:40 pm

Zaidi ya watoto elfu 86 kupata chanjo ya polio Rungwe

Halmashauri ya wilaya ya Rungwe inatarajia kuwafikia watoto zaidi ya elfu themanini na sita na kuwapatia chanjo ya polio ambayo imezinduliwa rasmi hii leo katika mikoa sita yenye hatari ya kupata ugonjwa huo hapa nchini. Na Sabina martin – RungweJamii…

21 September 2023, 4:08 pm

Milioni 362 kujenga stendi ya vumbi Tukuyu mjini

Kukamilika kwa stendi ya vumbi maarufu kama stendi ya Noah Tukuyu mjini itakuwa chachu ya maendeleo kwani itaondoa adha ya watumiaji wa stendi hiyo kwa msimu wa masika na kiangazi. Na Lennox Mwamakula – Rungwe-MbeyaJumla ya shilingi milioni 362 zimetengwa…

20 September 2023, 6:18 pm

Watoto elfu 34 kupatiwa chanjo ya polio halmashauri ya Busokelo.

watoto wenye mahitaji maalum pia wanahaki ya kupata hii chanjo ya polio hivyo msiwafungie ndani wapeni nafasi ya kupata chanjo. Na Sabina Martin – RungweWazazi na walezi katika halmashauri ya Busokelo wilayani Rungwe mkoani Mbeya wametakiwa kutowafungia watoto wenye mahitaji…

15 September 2023, 12:58 pm

Lumuli kuwamlika watoto yatima Rungwe

Jamii inatakiwa kuwalea na kuwalinda watoto yatima katika maeneo yao ikiwa ni pamoja na kuwalea katika mazingira yenye usalama kwao. Na Lennox Mwamakula Ili kukabiliana na wimbi la watoto waishio katika mazingira magumu uongozi wa kijiji na kata ya Ndanto…

13 September 2023, 1:16 pm

Wazazi, walezi watakiwa kuwa karibu na wanafunzi wakati wa mitihani

Wanafunzi wa darasa la saba wanatajia kufanya mitihani kote nchini hivyo jamii imeshauriwa kuwa sehemu ya watoto hao wakati wote ili wanafunzi waweze kufanya vizuri. Na Bahati Obel – Rungwe, Mbeya Wazazi na walezi wilayani Rungwe mkoani Mbeya wametakiwa kuhakikisha…

13 September 2023, 10:45 am

Kilimo cha strawberry chachu kwa wakullima wilayani Rungwe

Kutokana na wilaya ya Rungwe kuwa na kilimo cha mazao mbalimbali ya chakula, biashara, matunda na mbogamboga rai imetolewa kulima pia zao la Strawberry kutokana na zao hilo kustawi wilayani Rungwe mkoani Mbeya. Na Evodier Ngeng’ena – RungweWakulima wilayani Rungwe…

12 September 2023, 1:37 pm

Hatma ya watoto wa kike waliopata ujauzito katika umri mdogo

Mimba za utotoni ni miongoni mwa sababu zinazosababisha wasichana wengi kutotimiza ndoto zao huku takwimu zikionesha asilimia 40 ya wasichana huacha masomo kutokana na mimba, hii ni kwa mujibu wa utafiti wa mwaka 2016 wa Human Rights Watch. Frida Mwaipopo…

12 September 2023, 8:11 am

Kukosekana kwa wosia chanzo cha migogoro ya ardhi

Utamaduni wa watu wengi kutoandika wosia imetajwa kuwa chanzo cha migogoro ya ardhi katika jamii nyingi nchini Tanzania huku mila na desturi zikitajwa. Na Lennox Mwamakula- Rungwe Jamii imeshauriwa kuwa na utaratibu wa kuandika wosia ili kuondokana na mkanganyiko juu…

11 September 2023, 12:00 pm

CHADEMA: Wananchi washughulikie viongozi wazembe

Kuelekea uchaguzi mdogo wa serikali za mitaa 2024 vyama vya upinzani wameeleza mbinu watakazozitumia kuking’oa chama tawala madarakani. Na Cleef Mlelwa- Makambako Wananchi wa halmashauri ya mji wa Makambako wametakiwa kuwaondoa madarakani viongozi wote wa kisiasa ambao wameshindwa kutatua changamoto…

Kuhusu Chai FM

Chai FM radio ni radio inayomilikiwa na Umoja wa wakulima wa Chai Rungwe, Ilianzishwa kwa lengo la kuhakikisha mkulima wa Chai wilaya ya Rungwe anapata taarifa sahihi ambazo zitasaidia kuendeleza zao la Chai pamoja na shughuli zake za kiuchumi, Elimu na Kijamii.

Uwepo wa radio Chai FM umesaidia mkulima wa zao la Chai wilaya ya Rungwe kupata taarifa kwa wakati zinazohusu zao la chai na mwenendo wake pamoja na elimu juu ya kilimo biashara kwa zao la chai na mazao mengine pamoja na ufugaji.

Hii ni kutokana na uguu wa kufikisha taarifa ya masuala ya kilimo kwa wakulima wa chai jiografia ya wilaya ikiwa ni kikwazo kwa wakulima kupata taarifa mbalimbali za ndani na nje ya wilaya pamoja na mpango wa kilimo endelevu.

Dira

Kuona jamii ya wakulima na wafugaji wa wilaya ya Rungwe wanakuwa na maisha bora

Dhamira

Kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo wa ndani na nje ya Wilaya ya Rungwe kuelimisha na kutoa taarifa za kilimo, mifugo, biashara,viwanda na habari za kijamii kupitia vipindi vya redio.

Chai Fm Radio inasikika maeneo tofauti kama ifuatavyo

Mkoa wa Mbeya – Wilaya za Rungwe, Busokelo, Kyela, na Mbeya Vijijini kwa baadhi ya maeneo

Mkoa wa Njombe – Wilaya za Makete, Ludewa

Mkoa wa Songwe – Wilaya za Ileje na Songwe kwa baadhi ya maeneo

Mkoa wa Ruvuma – Wilaya za Mbinga na Nyasa.

Lakini pia chai Fm inapatikana ukiwa popote duniani kupitia radiotadio.co.tz/chaifm/