Hii ni shule ya Msingi Nuru iliyopo Kata ya Bagamoyo Tukuyu Mjini yenye mchepuo wa kingereza ambayo inatajwa kupanua maarifa na ujuzi kwa wanafunzi wa Wilaya Ya Rungwe
Kupitia Mapato ya shule hii pamoja na vyanzo vingine, Halmashauri imeweza kujenga na kusajili shule nyingine mpya kwa mchepuo wa Kingereza katika kata ya Kyimo (Umoja English Medium) na Ushirika Eng medium iliyopo kata ya Mpuguso.
Masomo katika shule hizi yanatarajiwa kuanza mapema mwezi huu wa Februari na Fomu za kujiunga zinapatikana katika shule hizi.
Fomu za kujiunga katika shule hizi zinaanza kutolewa siku ya Jumatatu tarehe 5.2.2024 na masomo yataanza kutolewa kuanzia siku hiyo.
Shule itakuwa na madarasa ya awali,kwanza na Darasa la pili.
Halmashauri kupitia Idara ya elimu Msingi tayari imeshapanga walimu kwa ajili ya usimamizi,uendeshaji pamoja na ufundishaji wa Wanafunzi.