Chai FM

Elimu ya sheria imeombwa kutolewa kwenye jamii ili kujenga uwelewa Rungwe

8 August 2024, 11:11 am

kutokana na jamii kutokuwa na uwelewa juu ya masuala ya sheria serikali inatakiwa kuweka utaratibu wa kuelimisha wananchi wake

RUNGWE-MBEYA

Na Gwamaka Mwakisyala

Ili kuhakikisha kuna kuwa na uwelewa wa sheria mbalimbali za nchi kwa wananchi,taasisi za kiraia na za umma zinazo simamia masuala ya sheria zimeomba kutoa elimu ya kisheria kwenye jamii

Kauli imetolewa na wananchi wilayani Rungwe wapokuwa wakizungumza na chaifm kwa nyakati tofauti juu ya uwelewa na umuhimu wa ulinzi wa taarifa binafsi baadhi wamesema wanao uwelewa kupita vyombo vya habari kuwa kila mtu anatakiwa kutunza taarifa zake bila kuingiliwa na mtu mwingine

sauti ya mwananchi

Kwa upande wake Ester John  na Hussen Mohmed wamesema sheria ya kulinda taarifa binafsi inasaidia kufanya mambo ya mtu kwa uhuru na kumjengea uwelewa juu ya masuala ya kisheria

sauti ya Ester na Hussen

Kwa upande wake Anna Julius ambaye ni mwanafunzi anaye soma taaluma ya sheria katika chuo kuu cha Dodoma mwaka wa tatu ameelezea umuhimu na na namna sheria hiyo ilivyo muhimu kwenye jamiii

sauti ya anna julius