Chai FM
Chai FM
5 May 2025, 2:50 pm

Katika kuelekea uchaguzi mkuu mwaka huu wanawake wametakiwa ushiriki kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya vyama vyao vya siasa
RUNGWE -MBEYA
Na Bertha Izengo
Wanawake nchini wametakiwa kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi wakati Taifa tunaelekea kwenye uchagaguzi mkuu October mwaka huu.
Kauli imetolewa na katibu wa chama cha mapinduzi wilaya ya Rungwe Abdallah Mpokwa alipokuwa kiongea na kituo hiki ofisini kwake amesema nafasi ya kugombea niyakila mmoja hivyo kama chama kinatoa fursa kwa wanachama wote bila kujali jinsia
Sauti ya katibu wa chama cha Mapinduzi wilaya
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtaa wa Bulyaga juu Ndg, Adam Mwaikonyole amesema kwa miaka ya hivi karibuni ushiriki wa wanawake kugombea nafasi mbalimbali kwenye vyama vya siasa unaongezeka siku hadi siku isipokuwa baadhi yao wakuwa nyuma kutokana na kushindwa kujiamini
sauti ya Mwenyekiti wa mtaa
Naye Lwitiko Mbughi kwa sasa wanawake wamepewa kipao mbele cha kushika nyazifa mbalimbali tofauti na hapo nyuma kutokana usawa ulipo kwenye jamii
sauti ya mwananchi
Aidha Ntuli Mwansasu ni moja wa wanawake ameeleza kuwa hapo awali wanawake hawakupewa nafasi kutokana mila na desturi zilizopo apo nyuma zilizo kuwa zikimdidimiza mtoto wa kike
sauti za wanawake