Chai FM

Wanufaika wa mikopo wafurahishwa Busokelo

11 February 2025, 11:24 am

RUNGWE-MBEYA

Mikopo ya serikali inawasaidia wananchi kujikwamua kiuchumi kwa ngazi ya familia na kuinua chumi wa halmashauri kwa ujumla.

Na Lennox Mwamakula

Zaidi ya  shilingi Milioni 177 zimetolewa na Halmashauri ya wilaya ya Busokelo kwa vikundi vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu ikiwa kwa awamu ya kwanza

Zoezi la uzinduaji wa utoaji wa mikopo kwa halmashauri ya busokelo limefanyika kata ya Ntaba mbele ya mwenyekiti ya halmashauri  mh, Anyosisye Njobelo  ambaye amewasihi wanufaika wa mikopo hiyo kwenda kuzifanyia kazi kwa malengo walio jiwekea

sauti ya mwenyekiti wa halmashauri

wanufaika wakikabidhiwa hundi ya mfano na viongozi mbalimbali wa serikali

Awali akisoma taarifa ya mikopo kaimu mkuu wa division ya maendeleo jamii wilaya Busokelo Ndg,John Kipingili amesema kabla ya utoaji wa mikopo hatua mbalimbali zilichukuliwa ikiwa ni utoaji wa elimu kwenye vikundi pamoja na kamati za mikopo ili kuvitambua vikundi vilivivyo kidhi vigezo

sauti ya afisa maendeleo 1

Hata hivyo kipingili amewaomba wananchi waliokosa kupata mikopo awamu ya kwanza waendele kuboresha taarifa zao na kuwatumia maafisa mikopo ngazi ya kata ili kupata elimu kujua vigezo vinavyo takiwa kwa wanufaika

Kaimu mkuu wa Division ya maendeleo ya jamii halmashauri ya Busokelo ndg,John Kapingili akisoma taaarifa mbele ya mgeni Rasmi

sauti ya afisa maendeleo 2

Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Busokelo Dr mwinyi omary  mwinyi  amewaomba wananchi kujitokeza kujisajili ili waweze kupatiwa fendha ili waweze kundelea kufanya shughuli zao za kujikwamua kiuchumi

wanufaika wa mikopo halmashauri ya busokelo

sauti ya mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Busokelo

Naye katibu tawala wa wilaya ya Rungwe Ndg Ally Kiumwa amesema hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa kikundi kitakacho sita kurejesha fedha hizo kwa muda uliopangwa

sauti ya katibu tawala

Kwa upande wao wanufaika wameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kuwapatia mkopo huo kwani wamesema fedha hizo zinakwenda kuwainua kiuchumi kwenye familia zao

sauti ya wanufaika