Chai FM
Chai FM
1 May 2026, 9:50 am

tuilinde amani ya nchi kuanzia ngazi ya familia na taifa kwa ujumla
RUNGWE-MBEYA
Na Lennox Mwamakula
Madiwani wilayani Rungwe wameombwa kupitia taarifa ya mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali ili kuweza kurekebisha makosa na changamoto zilizo bainishwa kwenye taarifa hiyo kwa lengo ya kuendelea kupata hati safi.
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Rungwe Mh, Jaffar Hanniu kwenye kikao cha Baraza la madiwani kwa kipindi cha Robo ya Tatu kuanzia January hadi March 2026 kilichofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Rungwe wa john Mwankenja amesema madiwani kuendelea kukusanya mapato ya ndani ndiyo msingi kuwezesha mipango ya maendeleo ya wilaya
Sauti ya DC 1
Mh, Hanniu amesema kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha amewaomba madiwani kutoa elimu kwa wananchi namna ya kukabiliana na mmomoyoko wa ardhi kwa kupanda miti ili kuweza kudhibiti madhara yanayoweza kujitokeza.
Sauti ya DC 2
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmshauri ya wilaya ya Rungwe Mh, Gabriel Mwakagenda amepongeza madiwani kwa ushirikiano wanaounyesha na kuwaomba kuendelea kudumisha amani kwenye kata na wasiwe chanzo cha kuanzisha migogoro ndani ya maeneo yao kutakwamisha maendeleo ya wilaya na Taifa kwa ujumla
Sauti ya Mwenyekiti wa Halmashauri
Pia Mwakagenda amemwagiza mkurugenzi mtendaji wa halmashauri kuandaa utaratibu ndani ya siku saba kwajili ya kamati ya fedha ili kupitia mradi ambao baraza limeagiza
Sauti ya maagizo
Renatus Mchau ni mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Rungwe ameliakikishia baraza kuwa yale yote yaliyo agizwa yanaenda kutekelezwa ili malengo ya halmashauri yaweze kufikiwa
Sauti ya mkurugenzi mtendaji