Chai FM
Chai FM
5 May 2025, 4:24 pm

serikali imeombwa kupunguza masharti ya kupata mikopo kwa vikundu vya vijana.wanawake na watu wenye ulemavu
RUNGWE-MBEYA
Na Neema Nyirenda
Baada ya serikali kufungua dirisha la mikopo awamu ya kwanza ya asilimia kumi ya halmashauri kwa vikundi vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu baadhi ya wana vikundi wilayani Rungwe vimelalamikia masharti yaliyowekwa namna ya kupata mikopo hiyo
Wakiongea kwa nyakati tofauti na ChaiFM baadhi ya vijana wamesema wameshindwa kupata mkopo kutokana na vigezo vilivyo wekwa na halmashaurii kwani inaonyesha serikali ilikuwa na malengo mazuri kwa wananchi wake ila kuna daadhi ya watumishi wana kwamisha watu kupata mikopo hiyo

Kaimu Afisa maendeleo ya Jamii wilaya ya Rungwe Israel Alimwene akiongea na wanahabari ofisini kwake
sauti ya kijana
Aidha naye Bi, Jestina Chaula ni mkazi wa Rungwe ameshangazwa na vitendo vinavyofanya na watumishi kuwazungusha bila mafanikio yoyote kwa madai kuwa hawezi kupatiwa mkopo kutokana na umri wake
sauti ya jestina chaula
Israel Alimwene nia afisa maendeleo ya jamii wilaya ya Rungwe amebainisha sifa za kikundi amesema kikundi ni lazima kiwe na katiba na kisajiliwe na hata shughuli zinazofanyika ndani ya kikundi husika zijulikane
sauti ya kaimu afisa maendeleo 1
Hata hivyo Alimwene amesema serikali imeboresha mikopo kwakutambua changamoto wanazo pitia watu wenye ulemavu nchini kwa kuwapatia mkopo wa mtu mmojammoja na si kwa vikundi .
sauti ya kaimu afisa maendeleo ya jamii 2