Chai FM

Wakazi Kisondela Rungwe wapeleka kilio cha maji kwa spika wa bunge

4 January 2024, 7:45 pm

Wananchi wakigalagala chini mbele ya spika wakiomba maji [picha na Lennox mwamkula]

Suala la maji limekuwa changamoto kubwa kwa wananchi wa wilaya ya Rungwe licha ya kuwepo kwa vyanzo vingi vya maji ndani ya wilaya hiyo.

RUNGWE-MBEYA

Na Lennox Mwamakula

wananchi wa Kijiji cha Kibatata Kata ya Kisondola Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya wamefikisha kilio cha maji mbele ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Tulia alipofanya ziara ya kikazi katika Kata hiyo.

wamesema changamoto kubwa wanayo kabiliana nayo wananchi tangu kuzaliwa kwao hajawai kuyaona maji safi na salama kitendo kinacho wapelekekea kutumia maji ya mito

sauti za wanachi wakilia juu ya maji

Kilio hicho kinaungwa mkono na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya Sophia Mwakagenda kupitia chama cha Demokrasia na maendeleo [CHADEMA] amesema kilio cha kazi hao kinatakiwa kufunyiwa kazi

Mh, spika wa Bunge la jamhuri ya Tanzania Tulia Ackson akizungumza na wakazi wa kata ya kisondela

sauti ya mwakagenda

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Mpokigwa Mwankuga amesema serikali inatekeleza miradi mbalimbali ukiwemo wa kata ya kisondela ambapo amesema utakapo kamili utaondoa kilio cha wananchi wa Kisondela na maeneo ya jirani

sauti ya mwenyekiti wa halmashauri

Naye Mtendaji Kata ya Kisondela Lusajo Kibona ametoa taarifa ya utekelezaji wa mradi wa maji ameioma serikali kukamilisha mradi huo kwa haraka ili wanachi waondokane na changamoto ya maji

sauti ya mtendaji wa kata

Kwa upande wake Spika wa Bunge Dkt Tulia Ackson amesema kilio hicho amekichukua kwa uzito mkubwa kinaenda kufanyiwa kazi

sauti ya spika wa Bunge la Tanzania

Naye Naibu Waziri wa maji Mhandisi Maryprisca Mahundi amewatoa hofu wananchi wa Kyela na Rungwe kwa serikali inaendelea na mkakati wa kulitumia Ziwa Nyasa kama chanzo kikubwa cha maji

Sauti ya Naibu waziri wa maji

Serikali imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji mikubwa na midogo ikiwemo ya uchimbaji wa visima ambapo kila mkoa umepatiwa gari la kuchimba visima.