Chai FM

Wananchi wametakiwa kushiriki kwenye mikutano ya kisheria Rungwe

5 May 2025, 5:27 pm

ili kujiletea maendeleo wananchi wanatakiwa kushiriki kwenye mikutano kawenye maeneo yao

RUNGWE-MBEYA

Na Derick Gwakisa

Wananchi wametakiwa kushiriki kwenye mikutano ya kimaendeleo  inayohitishwa na viongozi kwenye maeneo yao ili kupanga mikakati mbalimbali ya kimaendeleo

Wito huo umetolewa na afisa mtendaji wa kata ya msasani Julietha Sanga amesema maamuzi yote ya kimaendeleo yanatolewa na wananchi kwa kushirikiana na viongozi wao

afisa mtendaji wa kata ya Msasani Julietha sanga akiongea na mwandishi wa ChaiFm ofisini kwake

sauti ya afisa mtendaji kata ya msasani

Adam Mwenyekiti ni mwenyekiti  wa mtaa wa Bulyaga  amesema kuna umuhimu wa kushiriki kwenye mikutano ya mitaa,vijiji hadi kata waache kupuuza kwani wananchi ndiyo wenye kuleta maendeleo

sauti ya mwenyekiti wa mtaa

Mariam Igomole ni mkazi wa Tukuyu  amesema  suala la kushiriki kwenye mikutano inayohitishwa kwenye vijiji au mitaa ni muhimu kwani kunampa mwanachi  uelewa kuhusu mambo mbalimbali ya kijamii

sauti ya mariam Igomole

Naye  Derick mwalukasa amesema kwenye mikutano inayoitishwa ndiyo sehemu za kueleza changamoto zinazo wakabili kwenye maeneo yao ili kuweza kupata ufumbuzi wa kuzitatua

sauti Derick mwalukasa