Chai FM
Chai FM
30 May 2025, 9:49 am

wauguzi wakiwa kwenye maandamano kwenye siku ya kuadhimisha siku ya wauguzi Duniani [picha na Lennox Mwamakula]
Baada ya wauguzi kulalamikiwa madai yao serikali imeamua kushughulikia ili kuwawezesha kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa
Na Lennox Mwamakula
Tanzania ikiungana na mataifa mengine kuadhimisha siku ya wauguzi Duniani Mkuu wa wilaya ya Rungwe Mh.Jaffar Hanniu amewagiza wakurugenzi watendaji wa halmashauri zote za mkoa wa Mbeya na Taasisi zininge zinazo husika na masuala ya afya kushuguliki madai ya wauguzi na wakunga kabla ya mei 31 mwaka 2025.
Maagizo hayo yametolewa na mkuu wa wilaya Rungwe akimwakilisha mgeni rasmi mkuu wa mkoa wa Mbeya kwenye maadhimisho ya kusherekea siku ya wauguzi yaliyo addhimishwa kimkoa katika halmashauri ya Busokelo kwenye viwanja vya shule ya msingi Lwangwa

Awali akisoma risala mbele ya mgeni rasim katibu wa TANNA Bi, Kiliana Tulyanje amesema wauguzi wameendelea kufanya jidihada mbalimbali kuhakisha jamii ya watanzania inakuwa salama na afya njema
Hata hivyo Bi,Tulyanje amebainisha changamoto wanazo kabiliana nazo wauguzi ikiwa ni pamoja na uhaba wa wauguzi katika halmashauri mbalimbali zilimo ndani ya mkoa wa mbeya kutokana sera ya nchi na ilani ya chama cha mapinduzi ya kuwa na zahanati kwa kila kijiji
Hata hivyo wauguzi wametoa mapendekezo kwa serikali kuweka utaratibu wa kuwawezesha wauguzi wanapo kwenda kwenye makongamano mbalimbali na kuziamuru halmashauri kuweka umeme kwenye vituo vyote vyakutolea huduma za afya
Akijibu risala hiyo mkuu wa wilaya ya Rungwe amesema madai yanayo lalamikiwa na wauguzi yafanyiwe kazi kama yalivyo tolewa na Naibu waziri wa wizara ya utumishi ilivyotolewa akiwa mkoani Iringa ili wauguzi wandelee kufanya kazi zao bila malalamiko
Sambamba na hilo Mh,Hanniu amesema serikali imepokea suala la muundo wa utawala na mapitio ya sera ya afya ili wauguzi watambulike rasmi