Chai FM

Tamasha la DSW lawanufaisha vijana Rungwe

16 May 2025, 10:18 am

ili kukabiliana na vitendo vya ukatili nchini jamii imetakiwa kuwa mstari wa mbele kupinga vitendo hivyo

RUNGWE-MBEYA

Na Lennox Mwamakula

Wanaofanyiwa  vitendo  vya  ukatili kwenye jamii wanatakiwa kujenga utaratibu wa kutoa taarifa kwenye vyombo vya kisheria ili  waweze kupatiwa msaada wa kisheria.

Kauli hiyo imetolewa na Bupe Suka Polisi kata ya Mpuguso kwenye tamasha la michezo lililoandaliwa  na shirika lisilo la kiserikali la DSW lililofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Mpuguso iliyop kijiji cha Mpuguso kata ya Mpuguso amesema  vitendo vya  ukatili  vinaweza kukomeshwa iwapo jamii itaendelea kujenga utamaduni wa kutoa taarifa  na kuelimisha juu ya ukatili.

Sauti ya polis kata

Beata Mahenge ni afisa maendeleo kata ya Mpuguso  amesema kuwepo kwa matamasha hayo ya kutoa elimu juu ya vitendo vya ukatili  na elimu ya afya ya uzazi imesaidia kupunguza vitendo hivyo vya ukatili kwenye kata hiyo kwa kiasi kikubwa.

Sauti ya afisa maendeleo ya   jamii

Naye  Athuman  ni muuguzi kwenye kituo cha afya Mpuguso ametoa elimu ya afya ya uzazi kwa vijana ambapo amewasii vijana na jamii kwa ujumla kuwa na utaratibu wa kupima afya zao mara kwa mara ilikuwa na  afya Bora.

Sauti ya muuguzi

Baada ya kupatiwa elimi hiyo baadhi ya vijana wamesema elimu ya afya ya uzazi waliopatiwa wanakuenda kuwa mabalozi kwa vijana wengine

Sauti ya wanufaika

Victor Mwaipungu ni vijana kutoka  kikundi cha Mpuguso youth club ambaye ni miongoni mwalio elimu ya afya ya uzazi na kupinga vitendo vya ukatili  wameshukuru shirika la DSW kwa kuwajengea uwezo  na kuwa mabalozi kwa vijana wengine.

Sauti ya vijana

Mariam Abraham ni mratibu kutoka shirika la DSW amesema wanaandaa matamasha mbalimbali kwenye kata zilizopitiwa na mradi kwa lengo la kushirikiana na serikali kuhakikisha vitendo vya ukatili vinatokomezwa kwenye jamii.

sauti ya mratibu

Sambamba na hilo mratibu amesema ndani ya wilaya ya Rungwe mradi huo unatekelezwa kwenye kata kumi ana ametoa rai kuwa watu waliofika kwenye tamasha hilo kuwa elimu walioipata waweze kuisambaza kwenye jamii

Sauti ya mratibu 2