Chai FM

Wizara ya Kilimo kutatua kilio cha wakulima Rungwe

16 May 2025, 9:51 am

serikali kupitia wizara ya kilimo imekuja na mpango wa kusaidia amccos nchini

RUNGWE-MBEYA

Na Lennox Mwamakula

Mbunge wa viti maalum mkoa wa mbeya mh, Sophia Mwakagenda ameishukuru serikali kupitia wizara ya kilimo kwa kujenga Packhouse wilayani Rungwe mkoani Mbeya  ili mkulima wa zao  Parachichi aweze kupata soko la uwakika baada ya kuvuna

Ametoa kauli hiyo Mbele ya mkurugenzi mkuu wa  mamlaka ya udhibiti wa nafaka na mazao mchanyiko [COPRA] Irene Mlola kwenye ukumbi wa ofisi za  Amcos ya UWAMARU zilizopo kata ya kyimo wiliyani Rungwe  ambapo Mh, Mwakagenda amesema kwaniaba ya wakulima wa parachichi wanashukuru wizara ya kilimo kwa kuwaondolea madalaili kwa hao ndiyo wanao waumiza wakulima na kujinufaisha wao

Sauti ya Mh, Mwakagenda 1

Hata hivyo Mh, Mwakagenda amewaomba mkurugenzi wa COPRA kuboresha Barabara zinazotoka kwenye mshamba ili mkulima aweze kusafirisha mazao kwa urahisi,

Sauti ya Mh, mwakagenda 2

Dadi Sanga ni mkulima na  mwanacha wa UWAMARUameiomba serikali kuweka mazingira mazuri ya kusafirisha parachichi kwa kupitia Bandari ya Dar es salaam na Tanga ili tusiendele kutengemea Bandari za nchi jirani

Sauti ya mkulima

Naye Alfred Mwakasangula ni mjumbe wa Bodi ya umoja wa wakulima hao amemshukuru mbunge Sophia Mwakagenda kwa kuwakutanisha na Waziri wa kilimo nchini na amewaomba wakulima wenzake kujituma katika uzalishaji ili jitihata zinazofanywa na serikali ya kuwasaidia ziwe zenye tija

Sauti ya mjumbe

Aidha Mwenyekiti wa UWAMARU ndg,Edward Kabuje amesema lengo ya wizara kufika Rungwe ni baada ya kupeleka kilio chao hivyo Mamlaka ya udhibiti wa nafaka na mazao mchanganyiko imeona kunahaja ya kufika na kukutana na wakulima wa parachichi na kuwapatia elimu ya nmna ya uwendeshaji wa kilimo

Sauti ya Mwenyekiti