Chai FM

Kikundi cha mwanamke shujaa chamchangia Rais Samia Rungwe

6 May 2025, 5:21 pm

Kwa kutambua kazi zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jamii imeendelea kuungana na Dkt,samia kuendelea kuwatumikia wananchi kwa kipindi kingine cha miaka mitano ijayo

RUNGWE – MBEYA

Na Lennox Mwamakula

Mkuu wawilaya ya Rungwe Mh,Jaffar Hanniu amepokea kiasi ccha shilingi Milioni 1,132,200 kutoka kwenye kikundi cha Mwanamke shujaa kilichopo Tukuyu mjini zikiwa ni fedha kwaajili ya kuchangia Mhesshimiwa Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hasani ili aweze kuchukua fomu kwaajili ya kugombea Urahis mwaka huu 2025

Zoezi hilo la kupokea fedha hizo limefanyika kwenye ofisi za mkuu wa wilaya ya Rungwe zilizopo Tukuyu Mjini  mapema leo Mei 6/ 2025

Akikabidhi kwaniaba ya kikundi Mwenyekiti wa kikundi hicho Bi,Greda Mwakabumbe amesema wazzo la kumchangia Mh, Rais liliasisiwa  kwenye siku ya Mwanamke Duniani ambapo wana kikundi walianza kuchangia kidogokidogo mpaka kifikisha kiwango kicho cha fedha

Sauti ya Mwenyekiti 1

Bi,Mwakabumbe ameongeza kuwa wanakikundi wamefikia uwamuzi huo baada ya kuridhika na kazi ya kuboresha miundombinu ya Elimu,Aafya,Maji na barabara kwa kiwango kikubwa

Sauti ya Mwenyekiti 2

Kwa upande wake katibu wa kikundi hicho cha M wanawake Shujaa  Mwalimu  Elizabert Sekile kililicho wasukuma  sana ni namna rais Samia anavyo watumikia watanzania kwa moyo  wote

 Sauti ya sekile

Akipokea fedha hizo Mh, Hanniu amewashukuru wana kikundi hicho kwakuonyesha moyo wa kizalendo kwa taifa na kutambua kazi zinazofanywa na Rais wa Jamuhuri  wa muungano wa Tanzania wa kuwatumikia wananchi wake

Sauti ya Mkuu wa wilaya  Rungwe