Chai FM

Elimu kutolewa juu ya vitendo vya ukatili dhidi ya watoto Busokelo

30 July 2024, 3:47 pm

ASP Mstapher akitoa kwa wananchielimu juu ya vitendo ukatili

ili kukabiliana na vitendo ya ukatili kwenye jamii jeshi la polisi limeomba ushirikiano ili kuwabaini wanao fanya vitendo hivyo.

RUNGWE-MBEYA

Na Lennox mwamakula

Jamii  imeshauriwa  kutoa  ushirkiano  kwenye jeshi la polisi pindi jeshi hilo linapo fanya uchunguzi wa jambo lolote lililo kuwa na viashilia vya uvunjjifu wa amani

Kauli hiyo imetelewa na mrakibu msaidizi wa jeshi la polisi kituo cha polisi lwangwa kilichopo halmashauri ya Busokelo alipokuwa akitoa elimu juu vya vitendo vya ukatili vinavyo endelea kutokea kwenye jamii

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya busokelo Bi, loema peter akiwaomba wazazi na walezi kuwa karibu na watoto kutokana na vitendo vya ukatili

Elimu hiyo ameitoa kwenye mkutano wa hadhara uliyofanyika lwangwa mjini wakati wa ziara ya mbunge wa jimbo la busokelo ya kijiji kwa kijiji ya kusikilza kero za wananchi  ambapo mmoja ya wananchi aliwasilisha kero ya kuwa anashangazwa kusikia matukio kuwa vijana wa kiume wanaoana wenyewe kwa wenyewe na kusema kwanini wasichukuliwe hatua za kisheria

sauti ya mwananchi

Naye mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya busokelo Bi, Loema peter amesema kwenye jamii kuna wimbi kubwa la unyanyasaji wa kijinsia  watoto wanafanyiwa vitendo vya ukatili ikiwa ni kulawitiwa,hivyo amewaomba wazazi  kuwa makini na watoto

sauti ya mkurugenzi

Kwa upande wake mkuu wa kituo cha polisi lwangwa ASP Mstapher amesema wao kama jeshi la polisi wanapata taarifa za kuwapo kwa vitendo hivyo na wanawachukulia hatua wale wote wanaofanya vitendo hivyo  na kuwaomba wazazi wawe na utaratibu wa kuwaogesha watoto na kuwakagua

sauti ya ASP mstapher 1

Hata hivyo ASP Mstapher baadhi ya wazazi wamekuwa na utaratibu ya kutotoa taarifa kwenye vyombo vya kisheria na kumalizana kienyeji hiyo ameomba jamii kutoa ushirikiano pindi watu wanapo fanya vitendo hivyo visivyo kubarika kwenye jamii

sauti ya ASP mstapher 2