Chai FM

Mkandarasi apewa wiki tatu kukamilisha stendi Rungwe

4 June 2024, 5:14 pm

Ili kuboresha miundombinu wananchi wametakiwa kuwa mstari wa mbele kutoa ushirikiano kwa serikali pindi inapotekelezwa miradi mbalimbali kwenye maeneo yao

   RUNGWE-MBEYA

Na Lennox Mwamakula

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mh, Juma Homera  amemwagiza mkandarasi anayejenga stendi ya Mabasi Tukuyu kuikamilisha  ndani ya wiki tatu ili iweze kuanza kutumika

Homera ametoa maagizo hayo  alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa stendi hiyo ya mabasiinayo jengwa ndani ya halmashauri ya wilaya ya Rungwe katika mji mdogo wa tukuyu stendi ambayo imekuwa kilio cha muda mrefu cha wananchi

Mkuu wa koa wa Mbeya mh, Juma Homera akitoa maagizo ya utekelezaji wa stendi ya mabasi Tukuyu

Awali akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi mhandisi Eng, Omary Mataka amesema mradi huo umefikia asilimi 77 na pindi utakapo kamilika  wananchi  pamoja na wafanyabiashara watanufaika baada ya kuwekea mazingira rafiki ya kufanyia shughuli zao za kujingizia kipato

sauti ya mhandasi akisoma taarifa

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Rungwe Jaffar Hanniu akitoa salamu kwa niaba ya wananchi wa wilaya ya Rungwe amesema wananchi wanamshukuru rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha nyingi kwaajili ya miradi mbakimbali inayoendelea kutekelezwa ndani ya wilaya ikiwa ni pamoja na mradi ya elimu,afya na maji

Mkuu wa wilaya ya Rungwe Jaffar Hanniu akitoa pongezi mbele ya mkuu wa mkoa wa Mbeya kwa rais Samia kwa niaba ya wananchi wa wilaya ya Rungwe

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Rungwe Jaffar Hanniu

Akiongea mbele ya wananchi mkuu wa mkoa mh,Homera amesema kumekuwa na kusuasua kwa ujenzi wa stendi hiyo hivyo mkandarasi akishindwa kukamilisha kwa muda aliopewa hatua stahiki sitashukuliwa dhidi yake

wananchi wakiwa stendi ya mabasi tukuyu wakimsikiliza mkuu wa mkoa wa mbeya alipokuwa akitoa maagizo ya ukamilishaji wa stendi

Sauti ya mkuu wa mkoa Juma Homera 1

Hata hivyo Homera amewaomba wananchi kuachana na tabia ya kulalamika kuwa maisha magumu bali wajishughulishe  ka shughuli ndogondogo kwani amesema kutawasadia kujikwamua kiuchumi na amengeza kuwa serikali imeandaa utaratibu wa kutoa fedha za mikopo kwa mwananchi anaye jishughulisha

Sauti ya mkuu wa mkoa Juma Homera 2