Chai FM

Recent posts

26 January 2022, 8:50 am

Wananchi waitumie wiki ya sheria kupata msaada wa kisheria

RUNGWE-MBEYA Kuelekea kilele cha wiki ya sheria nchini mahakama wilayani Rungwe imewataka wananchi kujitokeza katika maeneo ambayo zoezi la utoaji elimu litakuwa likifanyika . Akizungumza na Radio Chai Kaimu Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Rungwe Bw.Augustine Lugome amesema  utaratibu huu …

3 January 2022, 9:46 am

Madarasa 24 yakamilikika kwa asilimia 100

RUNGWE-MBEYA Mkurugenzi  Mtendaji wa Halmashauri ya Busokelo Bi, LOEMA PETER  amekabidhi takribani vyumba vya madarasa 24 kwa Mkuu wa wilaya ya Rungwe  baada ya kumalika ndani ya muda ulio pangwa. Ametoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na kituo hiki huku akieleza…

24 December 2021, 5:45 am

Umbali chazo cha unyanyasaji wilayani Rungwe

Umbali wa malezi uliopo baina ya wazazi, walezi, walimu na watoto imetajwa kuwa moja kati ya sababu zinazopelekea kushamiri kwa vitendo vya unyanyasaji dhidi ya watoto wilayani Rungwe mkoani Mbeya. Aidha jamii imetakiwa kuwalinda zaidi watoto huku wazazi wakitakiwa kujenga…

16 December 2021, 2:27 pm

Vitabu zaidi ya elfu tatu vyapokelewa Rungwe

RUNGWE. Katika kuboresha mazingira ya elimu nchini wadau mbalimbali wa elimu wameshauriwa kusaidia vifaa mbalimbali kama vile vitabu vya kiada na ziada. Akizungumza mara baada ya kupokea vitabu kutokea taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Sakyambo interprisess yenye makao makuu yake…

14 December 2021, 5:14 am

Jamii iwatembelee watu wenye uhitaji

RUNGWE-MBEYA Wazazi na walezi wameaswa kuwajali  na kuwathamini watu wenye uhitaji kwa kutoa mahitaji muhimu kwa watoto hao ikiwemo kuwatembelea katika maeneo mbalimbali kwani itasaidia kuongeza faraja kwao. Hayo yamezungumzwa  na Umoja wa akina mama kutoka Katumba walipo watembelea watoto…

28 November 2021, 8:42 am

Serikali kutenga fedha kwajili ya kuboresha miundombinu ya maji Rungwe

RUNGWE-MBEYA Mbunge wa jimbo la Rungwe  ANTON  MWANTONA amesema tatizo la maji linalo wakabili wanachi wa jimbo la Rungwe linaenda kumalizika baada ya serikali kutenga fedha kwajili ya kuboresha miundombinu ya maji kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungunza na na…

28 November 2021, 8:37 am

Wizara ya Elimu itenge fedha kwajili ya  ukarabati wa shule kongwe nchini

RUNGWE-MBEYA Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania KASSIM  MAJALIWA ameagiza wizara ya Elimu kutenga fedha kwajili ya  ukarabati wa shule zote kongwe nchini. Maagizo hayo ameyatoa wakati alipofanya ziara ya kukagua miradi mbalimbali Mkoani Mbeya wilayani Rungwe Novemba…

23 November 2021, 9:34 am

TANLAP yawajengea uwezo wasaidizi wa kisheria Rungwe

RUNGWE Kaimu mkurugenzi kutoka mtandao wa Mashirika yanayotoa msaada wa kisheria Tanzania [TANLAP] MCHELELI MACHUMBANA ameitaka jamii kujua sheria mbambali ili kukabiliana na unyanyasaji uliopo kwenye maeneo yao. Ametoa kauli hiyo mbele ya wasaidizi wa kisheria waliopo wilayani Rungwe mkoani…

22 November 2021, 9:36 am

Mafunzo yawe chachu ya mabadiliko

RUNGWE-MBEYA NA:STAMILY MWAKYOMA Vijana wametakiwa kuwa vielelezo katika jamii kupitia mafunzo yanayotolewa na vyuo vya maendeleo ya wananchi hapa nchini. Kauli hiyo imetolewa na mgeni rasmi Ndugu Gerald Kimbunga  katika maafali ya 45 ya chuo cha maendeleo ya Wananchi Katumba…

15 November 2021, 3:09 pm

Jamii imetakiwa kusaidia watoto wenye uoni hafifu

RUNGWE-MBEYA Mwenyekiti wa chama wasioona (TLB )mkoa wa Mbeya ndg.YOHANA MONGA amewaomba wadau mbalimbali kote nchini kusaidia vifaa vya kufundishia watoto wenye mahitaji maalum mashuleni. Ametoa kauli hiyo alipokuwa akikabidhi fimbo nyeupe kwa wanafunzi wasioona kwenye shule ya mahitaji maalum…

Kuhusu Chai FM

Chai FM radio ni radio inayomilikiwa na Umoja wa wakulima wa Chai Rungwe, Ilianzishwa kwa lengo la kuhakikisha mkulima wa Chai wilaya ya Rungwe anapata taarifa sahihi ambazo zitasaidia kuendeleza zao la Chai pamoja na shughuli zake za kiuchumi, Elimu na Kijamii.

Uwepo wa radio Chai FM umesaidia mkulima wa zao la Chai wilaya ya Rungwe kupata taarifa kwa wakati zinazohusu zao la chai na mwenendo wake pamoja na elimu juu ya kilimo biashara kwa zao la chai na mazao mengine pamoja na ufugaji.

Hii ni kutokana na uguu wa kufikisha taarifa ya masuala ya kilimo kwa wakulima wa chai jiografia ya wilaya ikiwa ni kikwazo kwa wakulima kupata taarifa mbalimbali za ndani na nje ya wilaya pamoja na mpango wa kilimo endelevu.

Dira

Kuona jamii ya wakulima na wafugaji wa wilaya ya Rungwe wanakuwa na maisha bora

Dhamira

Kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo wa ndani na nje ya Wilaya ya Rungwe kuelimisha na kutoa taarifa za kilimo, mifugo, biashara,viwanda na habari za kijamii kupitia vipindi vya redio.

Chai Fm Radio inasikika maeneo tofauti kama ifuatavyo

Mkoa wa Mbeya – Wilaya za Rungwe, Busokelo, Kyela, na Mbeya Vijijini kwa baadhi ya maeneo

Mkoa wa Njombe – Wilaya za Makete, Ludewa

Mkoa wa Songwe – Wilaya za Ileje na Songwe kwa baadhi ya maeneo

Mkoa wa Ruvuma – Wilaya za Mbinga na Nyasa.

Lakini pia chai Fm inapatikana ukiwa popote duniani kupitia radiotadio.co.tz/chaifm/