Chai FM

Recent posts

18 March 2022, 9:19 am

Watumiaji wa barabara watakiwa kuzingatia sheria za usalama barabarani

RUNGWE Na Lennox Mwamakula Mkuu wa kikosi cha usalama Barabarani wilayani Rungwe mkoani Mbeya FELIX KAKOLANYA amewataka waendesha  vyombo vya moto kufuata sheria za barabarani wanapo tumia vyombo hivyo. Kauli hiyo ameitoa wakati akizungunza na madereva pamoja na watumiaji wengine…

16 March 2022, 11:11 am

Jicho la mama mkombozi wa watoto yatima na wasiojiweza Rungwe

RUNGWE, Na Sabina Martin Msaada wa mahitaji mbalimbali wenye thamani ya zaidi ya shilingi laki sita umetolewa kwa watoto yatima katika kituo cha kulelea watoto hao cha Igongwe wilayani Rungwe mkoani Mbeya. Mwenyekiti wa kikundi cha wanawake cha jicho la…

9 March 2022, 10:00 am

Siku ya wanawake duniani itumike kufikia jamii zenye uhitaji

RUNGWE-MBEYA NA:EZEKIEL KAPONELA Siku ya Mwanamke duniani leo imeadhimishwa katika Halmshauri ya Wilaya ya Rungwe huku ikitolewa misaada mbalimbali kwa wahitaji. Katika maadhimisho hayo yaliyokwenda sambamba na kauli mbiu isemayo “Kizazi cha haki na usawa kwa maendeleo endelevu”mamia ya wanawake…

23 February 2022, 5:21 am

Ruzuku kwa wakulima wa maparachichi itasaidia uzalishaji wa tija.

RUNGWE-MBEYA Mkuu wa walaya ya Rungwe Mkoani Mbeya Dkt VICENT ANNEY ameuomba uongozi wa  chama cha ushirika UWAMARU [AMCOS] kuwa na utaratibu wa kutoa ruzuku kwa wakulima wa maparachichi ili kuweza kuzalisha kwa tija. Ametoa kauli hiyo kwenye kikao cha…

22 February 2022, 8:41 am

Ubovu wa barabara kikwazo katika maendeleo

RUNGWE -MBEYA Wafanyabiashara pamoja na wakazi wa kijiji cha Mpandapanda kilichopo kata ya Kiwira wilayani Rungwe ambapo wameeleza namna wanavyoshindwa kufanya maendeleo ya kiuchumi kutokana na uharibifu wa miundombinu ya barabara. wakibainisha hayo baadhi ya wakazi pamoja na  wafanyabiashara wamesema…

21 February 2022, 9:45 am

Jamii yatakiwa kutowatenga wagonjwa wa fistula

RUNGWE-MBEYA NA:BETRIDA ANYEGILE Wito umetolewa kwa jamii wilayani Rungwe mkoani Mbeya kuachana na dhana potofu juu ya ugonjwa wa Fistula kwani ugonjwa huo unatibika bure bila mgonjwa kugharamia gharama yoyote. Akizungumza kwa njia ya Simu na Chai FM Program manager…

21 February 2022, 8:14 am

Malezi mabaya kwa watoto chanzo cha matukio ya uhalifu

RUNGWE-MBEYA Malezi mabaya kwa watoto wilayani Rungwe Mkoani Mbeya imeelezwa kuwa chanzo cha matukio mbalimbali ya uhalifu ikiwemo unyanyasaji wa kijinsia na mauaji. Ameyasema hayo Mch wa kanisa la Baptist Tukuyu mjini Mch. .HALLENCE MWASOMOLA, wakati akizungumza na redio chai…

20 February 2022, 5:08 pm

Wananchi wamshukuru Rais Samia fedha ujenzi shule ya sekondari

RUNGWE-MBEYA Umoja na ushirikiano  wa wakazi wa kata ya Msasani wilayani Rungwe umetajwa kuwa chanzo cha kumalizwa kwa ujenzi wa shule ya sekondari Msasani inayojengwa katika mtaa wa Bulongwe. Ameyasema hayo diwani wa kata ya msasani mh ROBIN MWAKAPESA, wakati…

16 February 2022, 10:03 am

Vijana wachangamkie mikopo ya halmashauri

RUNGWE-MBEYA. NA:JUDITH MWAKIBIBI Wananchi wilayani Rungwe mkoani Mbeya wametakiwa  kujiunga na vikundi mbalimbali ilikuweza kunufaika na mikopo inayotolewa na Halmashauri ikiwa ni vikundi vya watu wenye ulemavu ,wanawake na vijana. Akizungumza na redio Chai FM ofisini kwake Mratibu Wa Dawati …

Kuhusu Chai FM

Chai FM radio ni radio inayomilikiwa na Umoja wa wakulima wa Chai Rungwe, Ilianzishwa kwa lengo la kuhakikisha mkulima wa Chai wilaya ya Rungwe anapata taarifa sahihi ambazo zitasaidia kuendeleza zao la Chai pamoja na shughuli zake za kiuchumi, Elimu na Kijamii.

Uwepo wa radio Chai FM umesaidia mkulima wa zao la Chai wilaya ya Rungwe kupata taarifa kwa wakati zinazohusu zao la chai na mwenendo wake pamoja na elimu juu ya kilimo biashara kwa zao la chai na mazao mengine pamoja na ufugaji.

Hii ni kutokana na uguu wa kufikisha taarifa ya masuala ya kilimo kwa wakulima wa chai jiografia ya wilaya ikiwa ni kikwazo kwa wakulima kupata taarifa mbalimbali za ndani na nje ya wilaya pamoja na mpango wa kilimo endelevu.

Dira

Kuona jamii ya wakulima na wafugaji wa wilaya ya Rungwe wanakuwa na maisha bora

Dhamira

Kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo wa ndani na nje ya Wilaya ya Rungwe kuelimisha na kutoa taarifa za kilimo, mifugo, biashara,viwanda na habari za kijamii kupitia vipindi vya redio.

Chai Fm Radio inasikika maeneo tofauti kama ifuatavyo

Mkoa wa Mbeya – Wilaya za Rungwe, Busokelo, Kyela, na Mbeya Vijijini kwa baadhi ya maeneo

Mkoa wa Njombe – Wilaya za Makete, Ludewa

Mkoa wa Songwe – Wilaya za Ileje na Songwe kwa baadhi ya maeneo

Mkoa wa Ruvuma – Wilaya za Mbinga na Nyasa.

Lakini pia chai Fm inapatikana ukiwa popote duniani kupitia radiotadio.co.tz/chaifm/