Chai FM
Chai FM
27 March 2026, 3:54 pm
Uwepo wa mvua kumbwa zilizoambatana na upepo imesababisha vifo vya watu 20 huku idadi kubwa ya vifo ikiwa ni watoto.

Na Sabina Martin
Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya zimesababisha vifo vya watu 20 wengi wao wakiwa ni watoto ambao ni 15 katika kata tofauti za wilaya hii.
Hata hivyo mvua mbali na kusababisha vifo kwa wakazi hao wa Rungwe, imesababisha majeruhi ambapo baadhi ya walionusurika kuachwa bila makazi, huku baahi ya mazao ya liyokua shambani yakisombwa na maji.
Akizungumza na waandishi wa habari mkuu wa wilaya ya Rungwe Mh.Jaffar Hanniu ametoa rai kwa wananchi wa Rungwe wanaoishi katika maeneo hatarishi kuhama katika maeneo hayo ili kujikinga na madhara zaidi.
Idadi hiyo ya vifo imeongezeka kutoka vifo 18 vilivyoripotiwa hapo awali kufuatia vifo vya watu wawili katika kata ya Kinyala kitongoji cha Chunya kijiji cha Kipande.
Kata zilizoathirika zaidi na mvua hizi za masika ni pamoja na Kawetele, Ikuti, nkunga, lupepo na kinyala huku nyumba zaidi ya 10 zikiathirika na mvua hiyo.