Chai FM

Kiwango cha ufaulu chaongezeka Rungwe

3 July 2024, 6:20 pm

Ili kuwa na jamii yenye uelewa walimu wameshauriwa kuwa mstari wa mbele kutoa elimu bora kwa wanafunzi kwa lengo la kujenga kizazi chenye elimu

Rungwe-Mbeya

Na Bahati Obel

Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Jaffar Haniu amekemea tabia ya baadhi ya wakuu wa Shule  na waalimu wakuu  kudharau baadhi ya walimu  kwa kufanya maamuzi  wao pekeyao au na kundi lake la watu bila ya kushirikisha walimu wengine jambo ambalo linarudisha nyuma maendeleo ya taaluma katika shule .

Mkuu wa wilaya ametoa kauli hiyo alipokuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya elim katika halmashauri ya Rungwe yaliyofanyika katika ukumbi wa  Landmark hotel uliopo Tukuyu ambapo amesema jambo hilo linavunja molali ya walimu na kupelekea kuto kufanya vizuri katika baadhi ya maeneo na kumtaka mkurugenzi wa halmashauri pamoja na maafisa elim kuwakemea wakuu wote wa shule wenye tabia hizo.

walimu wakiwa kwenye maadhimisho ya elimu kwenye ukumbi wa landmark hotel tukuyu

sauti ya mkuu wa wilaya

Aidha Hanniu  ametumia nafasi hiyo  kuwataka wazazi  na walezi na jamii kwa ujumla kukemea vitendo vya ukatili kwa watoto  vinavyo endelea kutokea nchini ikiwa ni pamoja na ukatili kwa watu wenye ulemavu wa ngozi ambavyo vimeanza kujitokeza katika baadhi ya maeneo hapa nchini. (albino)kwa kusema kuwa vitendo hivyo havikubaliki na havitakiwi kutokea katika maeneo yetu

sauti ya mkuu wa wilaya 2

 Kwa Upande wake mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Rungwe Renatusi Mchau wamesema kutokana na shule zilizopo Rungwe kufanya vizuri kumekuwepo wa uhitaji mkubwa Kwa wazazi kuwahamishia watoto wao kwenye shule za Rungwe hivyo amewapongeza walimu Kwa kutoa elimu bora Kwa wanafunzi

sauti ya mkurugenzi

Awali katika taarifa ya utekelezaji wa  elimu msingi  katika  halmashauri ya Rungwe iliyosomwa na   afisa elimu msingi  Juma Mwajobe taarifa himetaja takiwimu za ufaulu Kwa kuzitaja shule 10 zilizofanya vizuri ndani ya Wilaya ya Rungwe na kubainisha changamoto zinazoikabili idara ya elimu msingi ikiwa ni pamoja na upungufu wa madarasa

sauti ya taarifa ya tathimini ya elimu

Siku ya elimu  Kwa wilaya ya Rungwe imeadhimishwa Leo julai 3 mwaka 2024 yenye kauli mbiu ‘ Tumedhamiliakutoa elimu bora inayolenga kumpa maarifa,ujuzi na maadili mema ikienda sambamba na utoaji tuzo kwa wanafunzi shule na walim waliofanya vizuri katika mitihani ya kitaifa.