Boma Hai FM

Kilosa yachota uzoefu Hai katika mfumo wa mawakala wa ukusanyaji mapato

3 September 2026, 1:57 pm

Pichani ni madiwani wa halmashauri ya wilaya ya kilosa wakiwa na kamati ya fedha ,uchumi na mipango ya halmashauri ya wilaya ya Hai. (Picha na Richard Salema)

Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro imepongeza namna Halmashauri ya Wilaya ya Hai inavyosimamia ukusanyaji wa mapato na miradi ya maendeleo, huku ikieleza kuwa matumizi ya mfumo wa mawakala yanaweza kusaidia kuongeza mapato na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Na Gervas Mosha

Hai – Kilimanjaro

Madiwani na wataalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro wameitembelea Halmashauri ya Wilaya ya Hai kwa lengo la kujifunza uzoefu wa halmashauri hiyo katika matumizi ya mfumo wa mawakala katika ukusanyaji wa mapato.

Ziara hiyo imefanyika Septemba 2, 2026, ambapo viongozi hao walipokelewa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai, Edmund Rutaraka, pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri  Dionis Myinga kabla ya kufanya kikao katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Hai.

Sauti ya mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Hai Edmund Rutaraka
Pichani ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Hai Edmund Rutaraka(aliyevaa miwani)pamoja na mkurugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya ya Hai Dionis Myinga wakiwa kwenye kikao katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya Hai pamoja na madiwani na wataalumu kutoka halmashauri ya wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro (hawapo pichani) picha na Richard Salema)

Akizungumza katika kikao hicho, Mhasibu wa Mapato wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai, Christopher Manzi, ameeleza namna mfumo wa mawakala unavyotumika katika ukusanyaji wa mapato, pamoja na sababu zilizoifanya halmashauri hiyo kuamua kutumia mfumo huo.

Sauti ya Mhasibu wa mapato wa halmashauri ya wilaya ya Hai Christopher Manzi

Baada ya kikao, madiwani na wataalamu  hao walipata  fursa ya kutembelea baadhi ya miradi ya maendeleo inayosimamiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Hai, ambapo walijifunza namna mfumo wa ukusanyaji wa mapato unavyotekelezwa kwa vitendo.

Pichani ni diwani wa halmashauri ya wilaya ya kilosa mkoani Morogoro (picha na Richard Salema)

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa  Vicent Lusinde ametoa shukrani na pongezi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Hai kwa namna inavyosimamia ukusanyaji wa mapato na utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kwamba wamejifunza .

Sauti ya makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Hai Vicent Lusinde

Akieleza katika ziara hiyo Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kilosa  Beatrice Mwinuka amesema kutokana na mafunzo waliyopata kutoka halmashauri ya wilaya ya Hai kuhusu mfumo wa mawakala katika ukusanyaji wa mapato utaisaidia halmashauri yake kuongeza kiwango cha mapato na hivyo kuiwezesha kutoa huduma stahiki kwa jamii ya wilaya ya kilosa

Pichani ni mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Kilosa Beatrice Mwinuka (Picha na Richard Salema)

Naye Diwani wa Kata ya Dumila wilayani Kilosa, Douglas Mwigumila, ameisifu Halmashauri ya Wilaya ya Hai kwa weledi katika usimamizi wa miradi ya maendeleo pamoja na ukusanyaji wa mapato.

Sauti ya diwani wa kata ya Dumila halmashauri ya wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro

Ziara hiyo inalenga kuwajengea uwezo viongozi na wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa kwa kujifunza uzoefu wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai katika kuboresha ukusanyaji wa mapato kupitia mfumo wa mawakala.