Boma Hai FM

Wagonjwa hospitali ya Kibon’goto waridhika na huduma

23 January 2024, 12:59 pm

Mkurugenzi mtendaji wa hospitali ya maalum ya taifa ya magonjwa ambukizi Kibon’goto akiwa na watumishi wa hospitali hiyo baada ya kukabidhiwa gari(picha na Elizabeth mafie)

Wagonjwa mbalimbali kutoka hospitali maalum ya taifa ya magonjwa ambukizi kibon’goto waridhishwa na huduma.

Na Elizabeth Mafie

Mkurugenzi mtendaji wa Hospitali maalumu ya Taifa ya magonjwa ambukizi Kibong’oto iliyopo wilayani Siha mkoani Kilimnjaro Dkt Leornad Subi  amesema hospitali hiyo itaendelea kuhakikisha wananchi wanahudumiwa vizuri bila kulalamika .

Dkt Subi ametoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza katika hospitali hiyo katika hafla ya uzinduzi wa mawili yaliyolewa na Serikali aina ya Land cruces yenye thamani ya shilingi milioni 400.

Kwa mujibu wa Dkt Subi,hospitali hiyo iliita watu kutoka nje kufanya utafiti  kuona wagonjwa katika hospitali hiyo wanaridhika na huduma  inayotolewa  katika hospitali hiyo ya Taifa ya magonjwa ambukizi

Dkt Subi amesema asilimia 97% ya Wagonjwa wanaopatiwa huduma kutika katika hospitali hiyo maalumu wanaridhika na huduma zinazotolewa na wataalamu katika hospitali hiyo. Hospitali ya Taifa ya magonjwa ambukizi Kibong’oto ni hospitali ya Taifa na inatumia sayansi  zaidi katika uchunguzi na ufuatiliaji  wa wagonjwa ndio maana zaidi ya aslimia 75 ya wagonjwa wanaotibiwa hapo wanapona na wanarudishwa nyumbani ndio kwamaana huduma ni nzuri zaidi.

Sauti ya Mkurugenzi mtendaji wa hospitali maalum ya taifa ya magonjwa ambukizi Kibong’oto Dkt Leornad Subi.