Boma Hai FM

Madiwani Hai wajifunza mbinu bora za kilimo Maonyesho ya Nanenane Arusha

10 August 2026, 9:19 am

Pichani niMkuu wa wilaya ya Hai Hassan Bomboko (katikati) na katibu tawala wa wilaya ya Hai Sospeter Magonera (kushoto) wakipewa maelezo kuhusu bidhaa kwenye maonyesho ya nanenane ( Picha na Riziki Lesuya)

Madiwani na wataalamu mbalimbali wa wilaya ya Hai wametembelea mabanda ya maonyesho nanenane yaliyopo katika viwanja vya Themi Jijini Arusha kujifunza na kujionea mbinu bora za kilimo na bidhaa za kilimo

Na Oliver Joel, Njiro-Arusha

Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro  Mheshimiwa Hassan  Bomboko, ametembelea mabanda mbalimbali katika maonesho ya 32 ya Kilimo, Mifugo katika  Sherehe za Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Themi Njiro jijini  Arusha.

Mheshimiwa  Bomboko ametembelea banda la halmashauri ya wilaya ya Hai agosti 6 2026 ambapo amepongeza tafiti na bunifu mbalimbali zinazofanywa na taasisi mbalimbali huku akitoa wito kwa wakulima na wafugaji walioshiriki maonesho hayo kuchukua mbinu mbalimbali za ufugaji na ukulima zitakazowawezesha kuboresha shughuli zao.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Hai Hassan Bomboko

Hata hivyo mheshimiwa Bomboko amewapongeza waandaaji wa maadhimisho ya nanenane na kuongeza kuwa mwitikio wa wananchi kujitokeza katika maadhimisho haya ni mkubwa ukilinganishwa na miaka iliyopita ,hivyo kuwataka wananchi wa Hai ambao ni wakulima na wafugaji kutobaki nyuma kushiriki katika maadhimisho hayo.

Kwenye picha ni bidhaa zilizopo kwenye banda la halmashauri ya wilaya ya Hai kwaajili ya maonyesho viwanja vya Themi jijini Arusha (Picha na Riziki Lesuya)

Aidha Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Hai Edmund Rutaraka ambaye pia ni diwani wa kata ya Muungano ameambatana na madiwani wa wilaya Hai  kutembeleamaonesho ya 32 ya Kilimo mifugo katika  Sherehe za nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Themi Njiro, Arusha.

Akizungumza  agosti 7 2026 mara baada ya kutembelea banda la halmashauri ya wilaya ya Hai na mabanda mengine,mwenyekiti wa halmashauri  amesema kuwa mbinu za kisasa walizojifunza zitawawezesha madiwani  kufikisha mbinu hizo za  kilimo na ufugaji kwa wananchi katika kata zao.

Sauti ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Hai na diwani wakata ya Muungano Mhe. Edmund Rutaraka

Naye Ruth Lyamuya ambaye ni mkurugenzi wa  Shalom products wanaojihusisha na usindikaji wa viungo vya chakula,viungo vya chai na  tiba lishe ambaye amepeleka bidhaa katika maonesho hayo ameishukuru halmashauri ya wilaya ya Hai kwa kuwawezesha kupata nafasi ya kutangaza bidhaa zao katika maonesho hayo.

Sauti ya mkurugenzi wa  Shalom products Ruth Lyamuya