Boma Hai FM
Boma Hai FM
4 September 2026, 7:00 pm

Jamii imetakiwa kuongeza ushirikiano na wadau wa elimu ili kuwafikia watu wazima ambao hawakupata fursa ya kusoma katika mfumo rasmi, huku elimu hiyo ikilenga kuwajengea ujuzi na maarifa ya kujikwamua kiuchumi na kuboresha maisha yao
Na Vaileth Silvester
Hai – Kilimanjaro
Jamii imetakiwa kushirikiana na wadau mbali mbali katika sekta ya elimu ili kuwezesha watu wazima waliokosa elimu katika mfumo rasmi waweze kunufaika na elimu ya watu wazima.

Katibu tawala wa mkoa wa Kilimanjaro, Yusuph Nzowa amebainisha hayo Septemba 4,2026 katika maadhimisho ya kilele cha juma la elimu ya watu wazima kimkoa yaliyofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Kibaoni wilayani Hai mkoani Kilimanjaro.
Nae Afisa elimu ya watu wazima mkoa wa Kilimanjaro Jacksoni Mtenga amesema pamoja na majukumu mengine, lengo kuu ni kuwawezesha wanufaika kupata elimu, ujuzi na kujikwamua kiuchumi
Baadhi ya wanufaika wa elimu ya watu wazima akiwemo Bi Christina Lolo na Bwana Hamisi Moka wameishukuru serikali kwa kuwawezesha kupata elimu ya kusoma, kuandika na kuhesabu kwani imewawezesha kuwa na uelewa wa mambo mbali mbali ikiwemo matumizi ya simu na maelekezo ya dawa.
Maadhimisho hayo yaliambatana na kutoa hati za pongezi kwa halmashauri na shule zilizofanya vizuri katika matokeo ya kidato cha sita.

Kaulimbiu ya maadhimisho ya kilele Cha juma la elimu ya watu wazima ni ” Kisomo kwa manufaa ya watu na ustawi wa jamii.”
