Boma Hai FM

Saashisha ahoji mgogoro wa Mrososangi na mwekezaji

23 June 2026, 1:32 pm

Pichani ni mbunge wa jimbo wa jimbo la Hai Saashisha Mafuwe(picha kwa msaada wa mtandao)

Serikali imesema itachukua hatua za kuvunja mkataba kati ya Chama cha Ushirika cha Mrososangi na mwekezaji husika endapo ujenzi wa kiwanda cha kuchakata parachichi hautatekelezwa kwa mujibu wa makubaliano yaliyowekwa.

Na Mwandishi wetu

Dodoma

Serikali imesema itavunja mkataba kati ya Chama cha Ushirika cha Mrososangi na mwekezaji husika iwapo mwekezaji huyo atashindwa kutekeleza wajibu wake wa kujenga kiwanda cha kuchakata parachichi kama ilivyoainishwa katika mkataba.

Sauti ya Naibu waziri wa Kilimo David Silinde

Kauli hiyo imetolewa Juni 22, 2026  na Naibu waziri wa Kilimo David Silinde wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Hai, ambapo amesema kuwa tayari serikali imemwandikia mwekezaji barua na inaendelea kulifuatilia suala hilo kwa ukaribu ili kuhakikisha ujenzi wa kiwanda hicho unatekelezwa kwa mujibu wa makubaliano.

Awali Mbunge wa Jimbo la Hai, Saashisha Mafuwe alihoji bungeni Dodoma akitaka kujua mpango wa serikali wa kutatua mgogoro uliopo kati ya mwekezaji na Chama cha Ushirika cha Mrososangi ili kuhakikisha masharti ya mkataba yanatekelezwa kikamilifu.

Sauti ya mbunge wa jimbo la Hai Saashisha Mafuwe