Boma Hai FM

Mashirika yasiyo ya kiserikali Hai yatakiwa kulinda mila na desturi za Kitanzania

21 May 2026, 3:01 pm

Pichani ni mkuu wa divisheni ya maendeleo ya jamii wilaya ya Hai Robart Mwanga(anaezungumza) kushoto ni Happness Eliufoo mwakilishi wa Nacongo wilaya ya Hai pamoja Adamu Mwashambo ambae ni mwakilishi wa Nacongo Taifa.(picha na Juma Robert)

Mashirika yasiyo ya kiserikali wilayani Hai yamehimizwa kuzingatia sheria, utamaduni wa Kitanzania na uwajibikaji wa kifedha wanapopokea ufadhili kutoka nje, ili kuhakikisha shughuli zao zinaendelea kuleta maendeleo chanya kwa jamii.

Na Juma Robert

Hai-Kilimanjaro

Mashirika yasiyo ya kiserikali wilayani Hai  mkoani Kilimanjaro yametakiwa kuhakikisha yanalipa ada kwa wakati pamoja na kulinda mila na desturi za Kitanzania wakati wanapopokea miswada kutoka katika mashirika ya nje yanayotoa ufadhili katika mashirika yao.

Wito huo umetolewa  Mei 16, 2026 na mkuu wa divisheni ya maendeleo ya jamii Wilaya ya Hai Robert Mwanga alipokuwa  mgeni rasmi kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Hai Hassan Bomboko katika mkutano wa   mwaka 2026  wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali uliofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya wilaya ya Hai.

Amesema kuwa yapo baadhi ya mashirika kutoka nje ya nchi yanayotoa ufadhili kwa kuweka masharti yanayokiuka mila na desturi za kitanzania  kama vile ushoga,hivyo ameyataka mashirika hayo kuepuka ufadhili huo kwani unaleta athari  katika jamii.

Sauti ya mkuu wa divisheni ya maendeleo ya jamii Wilaya ya Hai Robert Mwanga

Naye Elia Kapinga Mratibu wa mashirika yasiyo ya kiserikali wilaya ya  Hai ameyataka Mashirika yasiyo ya kiserikali kufuata kanuni na taratibu za kisheria ili kuweza kuleta maendeleo Chanya kwenye jamii.

Hata hivyo mwakilishi wa Nacongo taifa kutoka mkoa wa Kilimanjaro, Adam Mwashambo amepongeza mashirika hayo na viongozi wake kwa kufanya kazi nzuri ili kuhakikisha mashirika hayo yanaendelea kusonga mbele na kuwahasa kuwa wakurugenzi wa mashirika hayo kuendelea kudhuria mikutano kama huu.

Sauti mwakilishi wa Nacongo taifa kutoka mkoa wa Kilimanjaro, Adam Mwashambo

Kwa upande wake Mwakilishi wa Nacongo wilaya ya Hai Happynesss Eliufoo Kimaro ameyaomba mashirika yasiyo ya kiserikali kuwa na mpango mkakati wa kutembeleana na kufahamiana na kujengeana uwezo wa kupata maarifa tofautitofauti ili kuweza kuinuka katika masuala ya kupata fundi ili kuweza kujiendesha na kusaidia jamii.

Sauti ya mwakilishi wa Nacongo wilaya ya Hai Happynesss Eliufoo Kimaro