Boma Hai FM

Bodaboda Hai waonywa kubadili taa na milio ya pikipiki

15 May 2026, 11:50 am

Pichani ni Sajent Ramadhani Juma kutoka kituo cha polisi Boman’gombe kitengo cha usalama barabarani(picha na Elizabeth Mafie)

Bodaboda watakaobadili taa na milio ya pikipiki kukiona

Na Oliva Joel

Hai-Kilimanjaro

Maafisa usafirishaji maarufu bodaboda  wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro wameaswa kutokubadilisha mifumo ya milio na taa iliyowekwa katika pikipiki zao na kuweka taa zenye mwanga mkali  pamoja na kuweka milio yenye kelele kwani watakapobainika hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Wito huo umetolewa  Mei 15, 2026 na Sajent  Ramadhan Juma kutoka katika kituo cha polisi Bomang’ombe kitengo cha usalama barabarani alipokuwa akizungumza kupitia Redio Boma Hai Fm  katika kipindi cha Siku mpya.

Amesema kuwa kelele hizo zimekuwa adha kwa wananchi na watumiaji wengine wa barabara  huku akiwataka wale ambao wammebadilisha mifumo hiyo  kuirejesha katika hali ya kawaida kwani watakaobainika kukiuka agizo hilo watachukuliwa hatua kisheria ikiwa ni pamoja na faini na kupelekwa mahabusu  .

Sauti ya Sajenti Ramadhani Juma kutoka kituo cha polisi Boma’ngombe kitengo cha usalama barabarani.

Hata hivyo amewaasa madereva kuzingatia sheria za barabarani ili kuhakikisha kuwa wanakuwa salama wao wenyewe na watumiaji wengine wa barabara.