Boma Hai FM

Wafugaji Hai watakiwa kuzingatia kanuni za ufugaji kuepuka homa ya nguruwe

14 May 2026, 3:33 pm

Pichani ni Afisa Mifugo Halmashauri ya wilaya ya Hai Jackson Ishengoma akiwa katika kipindi cha siku mpya kinachorushwa na Radio Boma Hai Fm(picha na Anasta Urio)

Ili kuendelea kufuga kwa tija na kukuza kipato cha mtu mmoja mmoja, wafugaji wametakiwa kuzingatia taratibu na kanuni za ufugaji.

Na Anasta Urio

Hai- Kilimanjaro

Wafugaji wa Nguruwe wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro wametakiwa kufata kanuni na taratibu za ufugaji zinazotolewa na wataalamu wa mifugo ili Kuwaepusha na magonjwa kwa lengo la kufanya ufugaji wenye tija.

Hayo yamebainishwa afisa  mifugo wilaya ya Hai Jackson Ishengoma wakati akizungumza na Radio Boma Hai Fm kwenye kipindi cha siku mpya Mei  14 ,2026 alipokuwa akitoa elimu kuhusu ugonjwa wa homa ya nguruwe.

Ameeleza kuwa ugonjwa wa homa ya nguruwe ni hatari kwani unaua kwa haraka kutokana na virusi ambao wanaambukiza kutoka kwa wanya wa pori kuja kwa wanyama wa kufugwa na ugonjwa huo hauna chanjo hivyo ni vyema wafugaji  kuwa makini zaidi.

Aidha amesema kuwa kuna dalili zinazoweza kuonekana kwa nguruwe mara baada ya kupata ugonjwa huo ni pamoja na kuharisha  damu,kutapika,mimba kutoka ,na Nguruwe  kukosa nguvu ya kutembea hali inayoweza kusababisha kifo kwa nguruwe.

Sauti ya Jackson Ishengoma afisa mifugo wilaya ya Hai

Pia amesema kuwa ugonjwa huo unambukizwa kwa njia ya hewa na kuchangia chakula  hivyo amewaasa wafugaji kuzingatia usafi na usalama wa chakula cha nguruwe na ikitokea  ili kuwaepusha nguruwe kupata Ugonjwa huo.

Sauti ya Jackson Ishengoma afisa mifugo wilaya ya Hai