Boma Hai FM
Boma Hai FM
12 May 2026, 11:51 pm

Waalimu wa shule za msingi wilaya ya Hai wameaswa kukuza na kuibua vipaji vya wanafunzi mashuleni ili kujenga timu bora kwaajili ya mashindano ya kimkoa
Na Henry Keto, Hai-Kilimanjaro
Waalimu wa michezo mashuleni wametakiwa kujitoa kuinua na kukuza michezo katika wilaya ya Hai, ikiwa ni Moja ya sifa muhimu kwa walimu wa michezo mashuleni.
Wito huo umetolewa May 11,2026, na Mkuu wa idara ya Elimu ya awali na Msingi Musa Kalanje Wakati wa ufunguzi wa michezo (mitashumta) ilitofanyika katika uwanja wa Shule ya sekondari ya Hai day, wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, ambapo amewataka kuibua na kukuza michezo katika wilaya ya Hai na sio kuangalia tu upande wa Shule yake inayoshiriki kwenye michezo hiyo.
Pia amesema lengo la michezo hiyo ni kuunda timu ya wilaya itakayoshiriki na kuleta matokeo mazuri katika michezo kwenye ngazi ya mkoa wa Kilimanjaro, hivyo katika kuendesha mashindano hayo lengo liwe kuunda timu bora na sio kuangalia wanafunzi wa Shule au kata anayotoka peke yake, na hairuhusiwi kuingiza watu wengine tofauti na wanafunzi maarufu kama (Mamluki).

Kwa upande wake Afisa michezo wilaya ya Hai Faston Kagimbo ametoa wito kwa walimu ambao wapo kwenye Kamati ya kuunda timu nzuri kuangalia wale wenye uwezo wakuwakilisha mkoa kimichezo na asitokee mwalimu wakuhusika kuchagua mwanafunzi asiye na uwezo kwenye mashindano.
