Kitulo FM

Wananchi waomba bunduki, risasi kwa lengo la kufukuza ngedere waharibifu

22 July 2026, 10:04 am

viongozi wa kijiji wakiwa pamoja na diwani wa kata ya tandala kwenye mkutano wa kijiji

licha ya baadhi ya wananchi kupatiwa mafunzo ya kutumia bunduki wananchi wameiomba serikali kuwapa bunduki na risasi kwa lengo la kufukuza ngedere waharibifu wanaoharibu mazao yao shambani na kukosa mazao mengi ambayo walitarajia kuyapata na imekuwa ikiwaletea adha kubwa wakulima hao

na mwandishi wetu.

Kutokana na uharibifu wa mazao wanaoupata kutokana na uwepo wa ngedere, wananchi wa Kijiji cha Ihela wilayani Makete mkoani Njombe wameomba wananchi waliopewa mafunzo ya kutumia bunduki, wapewe bunduki na risasi wazitumie kufukuza wanyama hao

Wananchi hao wametoa kauli hiyo kwenye mkutano wa kijiji hicho wakati diwani wa kata ya tandala mhe ignatio mtawa alipokuwa akifanya ziara kijiji kwa kijiji kwa lengo la kusikiliza kero za wananchi

sauti za wananchi ihela

kulingana na ombi hilo la wananchi wa ihela Afisa Kilimo Kata ya Tandala Bruno Mhitche akatolea ufafanuzi jambo hilo akisema zoezi hilo ni la kutishia wanyama na si kuwaua, na pia utaratibu kwa sasa umebadilika

sauti ya afisa kilimo bruno

Naye diwani wa kata ya Tandala Egnatio Mtawa amewaeleza wananchi kuwa umiliki wa silaha sio jambo rahisi kama wanavyofikiri, na kwamba sheria za nchi kuhusu umiliki wa silaha zipo pale pale.

sauti ya diwani mtawa