Kitulo FM
Kitulo FM
4 June 2026, 9:41 am

Kutokana na kukubaliana kwenye vikao shuleni, wazazi wamewaasa wenzao wasiotoa michango pamoja na kuwatumia watoto wao kwenye utafutaji kuacha tabia hiyo.
Na Mwandishi Wetu
Wazazi pamoja na viongozi wa kijiji cha ivalalila kata ya iwawa wilaya ya makete wamesikitishwa na baadhi ya wazazi na walezi kushindwa kutoa michango ya shule baada ya kukubaliana katika mikutano
Hayo yamejiri hii leo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha ivalalila kata ya iwawa ambapo umehudhuriwa pia na mwenyekiti wa halmashauri ambaye pia ni diwani wa kata ya iwawa mhe Rabson mahenge pamoja na mwenyekiti wa mamlaka ya mji mdg wa iwawa ndg Joseph mbilinyi

Diwani wa kata ya iwawa ambaye pia ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya makete mhe Rabson Mahenge amewasii wazazi na walezi kutokufanya masihara kwenye swala la elimu na badala yake wajivunie kuwasomesha watoto wao kwamanufaa ya kwao na taifa kwa ujumla

Akizungumza mwalimu mkuu wa shule ya msingi ivalalila mwl Amina Kyando amekili kuwa na watoto ambao ni wasumbufu na watoro katika shule hiyo huku akieleza njia ambayo ametumia kwa baadhi ya wanafunzi watoro ili wasiweze kurudia jambo hilo
NAO baadhi ya wananchi waliohudhuria katika mkutano huo akiwemo jimines mahenge mkutano huo wamewasisitiza wazazi kuacha kuwaingiza watoto wao katika shughuli za utafutaji jambo ambalo limekuwa likisababisha utoro pamoja na watoto kushindwa kufanya vyema mitihani yao

Wakati huo huo diwani mahenge ameahidi kutoa kumpyuta katika shule ya msingi ivalalila itakayo wasidia walimu katika majukumu yao ya kazi ya kila siku
Nae mwenyekiti wa mamlaka ya mji mdg wa iwawa ndg joseph mbilinyi amewasiii wananchi wa ivalalila kuendelea kuwaheshimu viongozi waliowachagua pamoja na wataalAmu ambao serikali imewaletea