Kitulo FM
Kitulo FM
12 June 2026, 6:20 pm

mkuu wa wilaya ya makete pamoja na uongozi wa hospitali wakati wa kuwaona wagonjwa na kutoa vitu mbali mbali
watumishi wa hospitali ya wilaya ya makete wamepongezwa kwa utoaji wa huduma bora kwa wananchi wanapofika kwaajili ya kupata huduma na kuwasisitiza kuendela kutimiza majukumu yao kikamilifu
na omben mgongolwa
Mkuu wa Wilaya ya Makete, Mhe. Kissa Gwakisa Kasongwa, leo ametembelea na kuona wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya ya Makete, ikiwa ni pamoja na kujionea hali ya utoaji huduma.
Mhe. Kasongwa mara ya kuwatembelea wagonjwa, amewapongeza watumishi wa Hospitali hiyo kwa kutimiza majukumu yao kikamilifu na kuhakikisha utoaji wa huduma bora kwa wagonjwa.

mhe kissa kasongwa akikabidhi mfuko wa pampas hospitali ya wilaya ya makete
Aidha, Mhe. Kissa Kasongwa, amewasihi watumishi hao kuendelea kutoa huduma Bora kwa wagonjwa kwakuwa Serikali imewaamini, na imekuwa ikiendelea kuboresha utolewaji wa huduma za Afya ndani ya Wilaya ya Makete kwa kujenga miundombinu ya kisasa.

mkuu wa wilaya ya makete mhe Kissa akikabadhi baadhi ya vitu kwa mgonjwa
Kwa Upande wake, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Makete, Dkt. Ligobert Kalisa, amesema ziara ya Mkuu wa Wilaya Hospitalini hapo imeongeza hamasa katika utendaji kazi pamoja na kutambua umuhimu wa kada hiyo katika kuhakikisha Afya za wananchi zinaimarika.