Kitulo FM

Asilimia 14 ya watu wazima makete hawajui kusoma na kuandika

5 June 2026, 6:15 pm

afisa elimu ya watu wazima na elimu nje ya mfumo rasmi  ndg Babtisa Kaguo

kutokana na baadhi ya watu wazima kutokujua kusoma na kuandika halmashauri ya wilaya ya makete kupitia idara ya elimu ya watu wazima wameweka mikakati mathubiti ya kuweza kuhakikisha wakazi wote wa makete wanajua kusoma na kuandika

na mwandishi wetu

Imeelezwa kuwa asilimia 14 ya watu wazima wa Wilaya Makete Mkoani Njombe hawajui kusoma kuandika na kuhesabu

Hayo yamesemwa na Afisa elimu ya watu wazima na elimu nje ya mfumo rasmi  ndg Babtisa Kaguo alipokuwa akizungumza na kitulo fm  kuwa kutokana na kiwango hicho cha watu kutokujua kusoma kuandika na kuhesabu imewalazimu kuhakikisha wanatoa elimu kwa wananchi na kuelewa program zinazoendeshwa na elimu ya watu wazima katika halmashauri ya makete ili waweze kujitokeza na kujifunza.

Aidha ndg Kuguo amesema kuwa kwamujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 kuna wazazi hawajui kusoma kuandika na kuhesabu jambo linalowalizimu kuendelea kuhamasisha kujitokeza kwa wingi katika vituo vilivyopo ili waweze kujifunza kwa manufaa yao kwa ujumla

sauti ya kaguo 01

kaguo amesema mikakati waliyoiweka katika halmashauri ya wilaya ya makete ni  kuhakikisha asilimia 14 ya watu wazima wanajua kusoma huku akiongeza kuwa sera ya taifa ya elimu inasema kila shule ya msingi,sekondari ni kituo cha elimu ya watu wazima

sauti ya kaguo 02

afisa elimu ya watu wazima makete

kutokana na baadhi ya watu kuogopa kujiunga na mafunzo hayo kuhofia kunyanyapaliwa na familia au jamii, ndg kaguo ameeleza namna njia wanazotumia ili kuweza kuwapata watu hao na kupatiwa mafunzo yatakayo wasaidia kujua kusoma na kuandika,

sauti ya afisa elimu kaguo 3

Afisa elimu ameeleza tayari wataalamu wapatao sabini wapo ili kuweza kuhakikisha wanatoa elimu au mafunzo ya elimu ya watu wazima huku akiongeza kwa kusema kuwa baada ya kujua  kusoma na kuandika kuna kisomo cha manufaa kama kupata ujuzi wa kilimo cha viazi na mengine ili kuendelea kupata ujuzi zaidi

afisa elimu kaguo 4

Afisa elimu amesema mpango uliopo ni kuweza kuhakikisha ifikapo mwezi wa tisa mwaka huu halmashauri ya wilaya ya makete mkoani njombe kuwe na vituo zaidi ya therathini ambapo kwa sasa vipo vituo vinne vinavyotoa mafunzo hayo ya elimu kwa watu wazima