Kitulo FM

January 31, 2024, 7:56 am

Ded Makufwe akikabidhi vifaa vya shule kwa watoto walio katika mazingira magum Ipepo picha na Lulu Mbwaga

katika mwendelezo wa ziara za jukwaa la ustawi wa jamii Makete kutoa elimu ya malezi mkurugenzi mtendaji akiambatana na baadhi ya wataalam kutoka Halmashauri wametembelea kata ya Ipepo na kutoa msaada wa vifaa vya shule kwa watoto wanaotoka ktk mazingira Magum

na Lulu Mbwaga

Jukwaa la Ustawi wa mtoto la Wilaya ya Makete leo limetembelea kata ya Ipepo kwa ajili ya kutoa elimu ya malezi kwa wototo na kuwakabidhi vifaa vya shule kwa wanafunzi wanaoishi mazingira magumu

Wanafunzi hao wamekabidhiwa vifaa mbalimbali ikiwemo madaftari, kalamu, mashati, sweta ,viatu na mavazi mengine

miongoni mwa watoto waliokabidhiwa vifaaa

Akikabidhi vifaa hivyo mbele ya Kamati ya Maendeleo ya Kata (Kamaka) kata ya Ipepo Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Makete na Mwenyekiti wa Jukwaa la mtoto amesema vifaa hivyo vimetokana na michango ya wadau wa ndani ya Makete na nje ya Makete ambapo amewaomba wadau kuendelea kuchangia

Amesema lengo la jukwaa hili ni kutoa elimu na mahitaji kwa watoto ili waweze kupata elimu kwa kuwawezesha mahitaji muhimu na kuondokana na ukatili ambao unapelekea watoto kushindwa kumaliza masomo yao

Aidha amewaasa wanafunzi kusoma kwa bidii na kutumia vifaa hivyo walivokabidhiwa katika kuboresha taaluma yao kwa kufaulu vizuri darasani kwani Serikali ya awamu ya sita imeboresha na inaendelea kuboresha miundombinu ya shule

Mwalimu Thomas amesema jambo lililofanyika ni zuri na linawafundisha na kuwambusha kusaidia watoto ambao hawana mahitaji muhimu sambamba na hilo amemshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Makete kwa kuhamasisha na kuwa mstari wa mbele katika kuwakumbuka watoto

Akizungumza kwa niaba ya wanafunzi waliopata mahitaji hayo Ostela Sanga ameshukuru na kuahidi kuendelea kufanya vizuri katika masomo na kupewa vifaa hivyo vimeleta hamasa zaiadi ya kusoma kwa bidii

Jukwaa la ustawi wa mtoto linaongozwa na Mkurugenzi Mtendaji halmashaur ya Wilaya ya Makete na Leo limezindua zoezi la kutoa elimu ya malezi na kugawa vifaa vya shule katika kata ya Ipepo ambapo zoezi hili litafanyika Wilaya yote ya Makete