Kitulo FM
Kitulo FM
19 September 2026, 4:51 pm

pichani ni mkuu wa wilaya pamoja na mwenyekiti wa halmashauri kwenye zoezi la usafi hii leo
katika kuahakikisha mazingira yanakuwa safi katika mazingira yanayotuzunguka hii leo wananchi wameungana na mkuu wa wilaya ya makete katika kuhadhimisha siku ya usafi duniani kwa kusafisha mitaro ya maji jambo ambalo ni muhimu ili kuweza kuepukana na magonjwa na hata madhara ambayo yanweza kujitokeza wakati wa mvua ambazo zinatarajiwa kunyesha mwezi ujao
na mwandishi wetu
Mkuu wa Wilaya ya Makete, Mhe. kissa Gwakissa Kasongwa, amewataka wakazi wa Wilaya hiyo kuhakikisha kwa wanachukua tahadhari juu ya uwepo wa Mvua kubwa ya El Nino, kutokana na kuwepo kwa viashiria vya kuwepo kwa mvua hiyo kubwa kwa mujibu wa mamlaka ya hali ya hewa Tanzania TMA ambazo zinatarajiwa kuanza mwezi oktoba 2026.
Mhe. Kissa Kasongwa, amesema hayo leo Septemba 19,2026, wakati akiongea na wakazi Makete eneo la Soko kuu, mara baada ya Kushiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Usafi Duniani, ambayo yamefanywa kwa kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ya Kata ya Iwawa.
cue….. sauti ya kissa kasongwa

ni zoezi la usafi likiendelea kata ya iwawa
Katika kuhakikisha zoezi la usafi linazingatiwa kwa kiasi kikubwa mkuu wa wilaya mhe Kissa ameanzisha shindano ambalo litahusisha mitaa ndani ya kata ya iwawa ambayo itaweka mazingira safi pamoja na vyoo bora lakini pia soko lenye choo safi watapewa zawadi lengo ni kuendelea kuhamasisha usafi wa mazingira unazingatiwa kwa kiasi kikubwa katika makazi ya watu na hata kwenye maeneo ya biashara
Cue………saiti ya mhe kissa
Diwani wa kata ya iwawa ambaye pia ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya makete mhe Rabson Mahenge amemshukuru mkuu wa wilaya ya makete mhe Kissa Kasongwa pamoja na wananchi kwa kuungana pamoja katika kuweka mazingira safi kwa kuwa kata ya iwawa ni sehemu ambayo inapokea viongozi wengi hivyo ni jukumu la kuhakikisha mazingira yanakuwa safi ili kuweza kuvutia wageni wanapokuja kutembelea wilaya ya makete
Cue…..sauti ya diwani mahenge

mkuu wa wilaya akizungumza na wananchi baada ya usafi
Mkuu wa kitengo cha udhibiti wa taka na usafi wa mazingira Omari Khamis amesema kuwa kuwa leo ni siku ya usafishaji duniani ambayo ilitangazwa pia na umoja wa mataifa (UN) hivyo ni jukumu la kila mwananchi kuweza kuhakikisha mazingira yanakuwa safi huku diwani viti maalumu Anifa sanga akiwashukuru wananchi kwa kujitokeza kwenye zoezi hilo la usafi
Cue……sauti ya khamis vs anifa
Nae mwenyekiti wa mamlaka ya mji mdogo wa iwawa ndg Joseph mbilinyi amewapongeza wananchi kwa kujitokeza kwa wingi kwenye shughuli ya usafi huku akiwasisitiza kuwa zoezi hilo la usafi linatakiwa kuwa endelevu na hata kwenye makazi yao ya kila siku
Cue…………sauti ya joseph mbilinyi

dc makete azungumza na wananchi
Nao baadhi ya wananchi walioshiriki zoezi la usafi akiwemo imelda sanga wamepongeza kwa jitihada hizo za kuhakikisha mji wa iwawa unakuwa safi huku wakiwataka wananchi kuacha tabia ya kutupa pampas kwenye mitaro ya mifereji kwakuwa inaweza kusababisha magonjwa ya mlipuko kuweza kutokea
Cue…………sauti ya wananchi

wananchi wakimsikiliza dc makete baada ya kumaliza shughuli ya usafi
Siku ya Usafi Duniani ilianzishwa mwaka 2023 na Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kama siku ya kimataifa inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 20 Septemba ambapo kwa wilaya ya makete imeadhimishwa hii leo septemba 19,2026