Pangani FM
Pangani FM
10/03/2026, 19:12

“Tunalishukuru shirika la UZIKWASA kwa kutupa mafunzo haya ya udhibiti wa taka, kwakuwa yametusaidia kutengeneza mkaa mbadala kupitia maganda ya ndizi kwasasa mazingira yetu ni safi”
Na Cosmas Clement
Baadhi ya vijana kutoka vijiji vya wilaya ya Pangani wamelipongeza shirika la Uzima Kwa Sanaa (UZIKWASA) kwa kuwawezesha katika kuchukua hatua ya udhibiti wa aina mbalimbali za taka katika maeneo yao.
Wakizungumza hii leo wakati wa zoezi la tathimini ya mafunzo ya udhibiti taka, vijana hao wamesema mafunzo hayo yamewawezesha kuzitumia taka kutengeneza bidhaa mbalimbali hivyo kuwaingizia kipato.
Bi Gladnes Mgendi ambaye ni afisa vijana wilaya ya Pangani pamoja na kuwapongeza shirika hilo pia amewataka vijana kutokuwa na hofu katika kuziendea fursa zilizopo kupitia taka.
Naye mwezeshaji kutoka shirika la UZIKWASA Bi Salvata Kalanga amewaasa vijana hao kuendelea kuwa mabalozi wazuri kwa kuhamaisha usafi wa mazingira katika maeneo yao.
UZIKWASA kifupi cha Uzima Kwa Sanaa ni shirika lisilo la kiserikali lenye makao yake wilayani Pangani limekuwa likitoa mafunzo ya mazingira kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuchukua hatua dhidi ya athari za mabadiliko ya tabia nchi.