Pangani FM

Pangani kuja na mkakati kabambe wa usafi

4 June 2024, 2:34 pm

Kutoka kulia mwenye shati jekundu ni Mdhibiti Taka na Usafi Wilayani Pangani Bwana Daniel Kijazi, katikati ni mkuu wa idara ya maliasili wilaya ya Pangani bwana Twahiru Mkongo na wa mwisho kushoto ni bwana Daudi Mlahagwa afisa mazingira wilaya ya Pangani.

Ni zaidi ya muongo mmoja umepita bila ya uwepo wa utatibu wa mdhabuni wa ukusanyaji taka hivyo kupelekea changamoto ya taka kuzaga katika mji wa Pangani kujaa.

Na Saa Zumo

Halmashauri ya wilaya ya Pangani imesema inaandaa mpango wa kudhibiti Taka kwa kutafuta mdhabuni atakaye zikusanya na kuzipeleka Dampo ili kuimarisha usafi wa mazingira katika halmashauri hiyo.

Hayo yameelezwa na Mdhibiti Taka na Usafi Wilayani Pangani Bwana Daniel Kijazi wakati akizungumza na kituo hiki na amekiri uwepo wa changamoto ya kuzagaa kwa taka kutokana na kukosekana miundombinu rafiki ya kuzikusanya.

Mdhibiti Taka na Usafi Wilayani Pangani Bwana Daniel Kijazi

Kwa upande wake Afisa Mazingira Wilaya humo Bwana Daud Mlahangwa amesema shughuli za kibinadamu ikiwemo kilimo husababisha uchakavu wa ardhi hivyo jamii inawajibu wa kuitunza kwa kupanda miti.

Sauti ya afisa mazingira wilaya ya Pangani bwana Daudi Mlahagwa

Naye Mkuu wa kitengo cha Maliasili Bwana Twahiru Mkongo akaisihi jamii wilayani PANGANI kutilia mkazo uhifadhi na utunzaji wa mazingira kwa maslahi ya afya zao na kuishi maeneo yaliyo salama.

Sauti ya Bwana Twahiru Mkongo

Hayo yamejiri ikiwa Kesho Juni 5 ni maadhimisha ya kilele cha siku ya Mazingira duniani ambapo Halmashauri ya wilaya ya Pangani mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Mkuu wa wilaya ya Pangani MUSSA KILAKALA na Kauli mbiu yake kwa  mwaka huu 2024 ni ‘’urejeshwaji wa ardhi na ustahamilivu wa hali ya jangwa na ukame.’’