Pangani FM
Pangani FM
19 March 2026, 23:39

“Tunaomba maafisa maendeleo ya jamii kata zote kutoa ushirikiano na wilaya tunaomba muwe na kipaumbele kusimamia mradi huu” Bi Oliver
Na Cosmas Clement
Wawakilishi kutoka Ubalozi wa Ireland nchini Tanzania wamesema wameridhishwa na utekelezaji wa mradi wa kuongeza uwezo kwa vikundi vya kijamii katika halmashuri ya wilaya ya Handeni unaoendeshwa na shirika la UZIKWASA lenye makao yake wilayani Pangani.
Wawakilishi hao wameyasema hayo hii leo wakati wa ziara ya kupitia na kutathimini maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo wenye lengo la kuwezesha vikundi hivyo vya kijamii wilayani Handeni kufikia usawa wa kijinsia na mabadiliko ya tabianchi.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo meneja wa mradi Bi Oliver Kinabo kutoka ubalozi wa Ireland, amelipongeza shirika la UZIKWASA kwa kuwezesha vikundi mbalimbali vya wanawake na vijana ambavyo vimekuwa ni chachu ya mabadiliko katika jamii yao.
Akiongea kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Handeni ambaye ndiyo alikuwa mgeni rasmi, kaimu mkuu wa wiaya hiyo Bwana Lugaila Nkwabi amewataka watendaji na maafisa maendeleo ya kata zinazotekelezwa mradi huo, kusimamia kikamilifu utekelezaji wa mradi huo ili kufikia mafanikio yanayolengwa.

Kwa upande wake mwezeshaji kutoka shirika la UZIKWASA bwana Erick Malya amesema kupitia mradi huo vikundi mbalimbali vilivyopo kata tano vimejengewa uwezo ili kuwezesha wanawake na vijana kiuchumi ili kukabiliana na matukio ya ukatili na athari za mabadiliko ya tabia nchi.
Katika ziara hiyo Shirika la UZIKWASA na wawakilishi kutoka Ubalozi wa Ireland wamekutana na wakuu wa idara na wakuu wa vitengo mbalimbali pamoja na mwakili wa mguu wa wilaya ya handeni ili kutathimini maendele ya mradi huo.
UZIKWASA ni shirika lisilo la kiserikali linalojihusisha na kuwajengea uwezo wnajamii katika kuchukua hatua za usawa wa kijinsi na mabadiliko ya tabia nchi.