Pangani FM

Soko lililokwama kwa zaidi ya miaka kumi, sasa kukamilika kwa miezi isiyozidi sita

12/03/2026, 21:27

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tanga na MCC Mhe. Rajabu Abdulrahman akiwa katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo wilaya ya Pangani.

Huku ni kuwarudisha nyuma wananchi na kuwavunja moyo waliacha kazi zao na kuchimba msingi wakiamini wanatengeneza kitu cha kuwasaidia lakini mpaka sasa malengo hayajatimia, lazima tuwasaidie wananchi kutatua changamoto zao, soko hili likikamilika wananchi wataongeza kipato chao na hayo ndiyo malengo ya chama cha mapinduzi.

Na Cosmas Clement

Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi mkoa wa Tanga MCC  Rajabu Abdulrahman ameamuagiza Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Pangani, ujenzi wa soko la Pangani Magharibi uliosimama kwa zaidi ya miaka kumi unakamilika haraka ili wananchi wapate sehemu nzuri ya kufanyia biashara.

Agizo hilo amelitoa March,12,2026 katika ziara yake alipotembelea miradi ya soko hilo pamoja na stendi ya daladala ya mji wa Pangani na kutoa kiasi cha shilingi milioni kumi kwa ajili ya kukamilisha mradi wa soko hilo.

Sauti ya MCC Rajabu Abdulrahman

MCC Rajabu ametaka soko hilo likamilike na kuanza kazi ifikapo mwezi wa tisa mwaka 2026 ili wananchi walitumie kwa ajili ya shughuli za kiuchumi.

Muonekano wa soko la Pangani Magharibi wilaya ya Pangani katika picha wakati wa ziara ya MCC Rajabu Abdulrahman
Sauti ya MCC Rajabu Abdulrahman

Ameagiza kuchukuliwe hatua madhubuti za kuzuia changamoto ya maji katika eneo hilo na kuanza kuhamasisha wafanyabiashara kuchukua maeneo ya kufanyia shughuli zao pamoja na kuweka utaratibu wa gulio.

Sauti ya MCC Rajabu Abdulrahman

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya kijiji cha Pangani Magharibi inadaiwa kuwa Ujenzi wa soko hilo hapo awali ulianzishwa mnamo mwaka 2007 kupitia mradi wa TASAF na kutumika kiasi cha shilingi milioni 29  hata hivyo ujenzi wake ulisimama huku wananchi wakihusika katika kuchimba msingi wa soko hilo.